Ticker

6/recent/ticker-posts

DC MONDULI AENDESHA ZOEZI LA UKAMATAJI WATOTO MINADANI

 
 Mkuu wa Wilaya ya Monduli, Francis Miti.
Na Woinde Shizza,Monduli


Imeelezwa kuwa Asilimia 10 ya watoto wilayani Monduli wanatajwa kutokwenda shule kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo utoro,pamoja na kufanya biashara katika  baadhi ya minada wilayani humo jambo ambalo limeamsha hisia za viongozi wa wilaya na kuamua kufanya operesheni ya kuwakamata na kuwapeleka shule kwa lazima Zaidi ya watoto 21.
 
 
 
Hayo yameelezwa leo naAfisa elimu msingi Theresia Kyala kutoka wilaya ya Monduli  mara baada ya ya zoezi la ukamataji wa watoto watoro amnao wanafanya biashara eneo la minada ambapo zoezi hilo lilifanyika mnada wa katika eneo la losirwa   iliyoko  kata ya mto wa mbu iko ambapo  ni utekelezaji wa agizo la Mkuu wa wilaya ya Monduli bw,Francis Miti ambapo eneo hilo lina  wakazi laki tatu kwa mujibu wa sensa ya mwaka 2012 huku Zaidi wakiwa ni wakazi wa jamii ya kifugaji.


Ambapo zoezi hilo limeendeshwa chininya usisamizi wa mkuu huyo na uongozi wa idara ya elimu   imetembelea eneo la  mnada wa Kigongoni na kuona watoto namna ambavyo wanaendelea kufanya biashara ndani ya mnada huo wakati wenzao wakiwa madarasani ambapo nikazungumza na baadhi ya watoto hao ambao wanaelezea baadhi ya sababu zilizowapelekea kutokwenda shule ikiwemo ugumu wa maisha huku wengine wakishindwa kujielezea.
 
 
Theresia Kyara ni afisa elimu msingi wilayani Monduli alisema  kuwazoezi la  operesheni hiyo wameianza rasmi katika soko la Alhamisi la eneo la monduli mjini na kufanikiwa kukamata watoto 16 na leo hii wamekamata watoto 21 hii kati ya hao watoto sita wamepelekwa bweni shule ya Manyara inaongeza idadi ya watoto ambao hawajaenda shule katika wilaya hiyo.

Kwa upande wake mkuu wa wilaya hiyo ya Monduli Francis Miti amesema kuwa ameamua kutoa agizo hilo na kutekelezwa kwa lengo la kuwawezesha kwa kila mtoto mwenye sifa ya kwenda shule aweze kupata elimu hiyo ya kuanzaia msingi bure kwa lengo la kumuunga mkono mh,Rais katika utoaji wa elimu bure ili kuweza kuweza kushinda katika sekta ya elimu.

Pia amewataka wazazi wote wenye watoto kuhakikisha wanapeleka shule watoto wao na kuwaandikisha na endapo mzazi ama mlezi atakae mhusisha na kumkataza mtoto wake hatua za kisheria zitachukuliwa.

 Mkuu wa wilaya ya Monduli ameongeza kuwa zoezi hili la ukamatwaji wa watoto hao ambao kati yao wapo waliotoka kwaajili ya kuchunga katika minada huku wengine wakiwa hawajasoma kabisaa.

Nae mmoja  wa mzazi bi,Moses ole laizer  amesema  kuwa zoezi hilo la kukamata watoto hao litaleta tija katika jamii kutokana na kuwa hakuna sababu inayofanya watoto hao wasiende shule kutokana na elimu kuwa bure na wazazi kuwaachia baadhi yao kuenda kufanya biashara minadani.
 
 Aliongeza kuwa baadhi ya Jamii za kifugaji  hususani wamasai wamekuwa na muamko mdogo wa kupeleka watoto wao kupata elimu jambo ambalo linawanyima haki ya msingi kwa kila mtoto mwenye sifa kwenda shule

Post a Comment

0 Comments