Ticker

6/recent/ticker-posts

POLISI:HATUHOFII KUMHOJI AU KUMKAMATA MAALIM SEIF


Na Mwandishi Wetu, Zanzibar
Jeshi la Polisi Zanzibar limesema haliogopi kumhoji au limeshindwa kukamkata Katibu Mkuu wa Chama Cha a2ananchi  (CUF ) Maalim seif sharif Hamad na kwanba limeahirisha tubkufanya hivyo jana ila dhamira bado iko pale pale ya kumhoji  na kumtaka atoe maelezo husika.
Aidha jeshi hilo limesisitiza kuwa linaweza kukamata kiongozi yeyote wa kisiasa wmbaye hana kinga za kisheria kwa ajili ya mahojiano,kumtaka atoe maelezo au ufafanuzi kuhusiana na masuala kadhaa yanayotia shaka .
Naibu Mkurugenzi  wa Makosa ya jinai zanzibar kamanda Salum Msangi amethibitisha hayo jana baada ya jeshi hilo kuahirisha kufanya naye mahojiano hadi itakaoopanga tena haraka toka sasa.
Kamanda Msangi elisema wanaofikiri kuwa polisi wameshindwa au wanakuogopa kumhoji kiongozi hiyo hawana hoja ya msingi huku akisema kuwa kutokana na miingiliano ya kimajukumu ndiko kulikofanya mahojiano hayo yaaihirishwe.
"Tumeahirisha kumhoji kutokana na muoingiliqno ya majukumu yetu ya kipolisi na si kumhofia su kumuogopa, tukitaka kumhoji jumanne akaonba ahijiwe ijumaa  (jana)ambapo nasi kutokana na sababu za kiutendaji tumeoanga kuwita wakati mwingine "alisema .
Aidha Naibu huyo Mkurugenzi wa Makosa ya Jinai alisema si muda mrefu toka sasa jeshi hilo kutamwita kiongozi huyo wa upinzani ili kumhoji kutokana na masuala kadhaa ambayo bado yako kwenye mabano.
Alipiulizwa kutikana na kitendo cha polisi mara kadhaa kukamata waziri wa zamani wa smz kumhoji na kushindwa kumfikisha mahakamani kujibu mashitaka yanayomkabili, Kamanda Msangi alisema kukanatwa au kuhojiwa na polisi haina maana unakabiliwa na shitaka au kesi mahakamani.
"Tuna uwezo kisheria kumwita mtu tunayemtuhumu kwa sababu kadhaa kituhuma ili kuchukua maelezo yake,kuhitaji ufafanuzi toka kwake baadae aidha kumfikisha mahakamani au kumwachia huru hadi wakati muafaka "alieleza kamanda huyo .
Jeshi la polisi mapema wiki yq jana kilisema limemeita katibu mkuu wa cuf maalim seif ili kumhoji kwa msuala kadhaa jambo ambalo hadi sasa mahijiano hayo yamekwama kufanyika.
Macho na masiko ya wengi wanatia shaka huenda kiongozi huyo kuitwa kwake polisi ni kufuatia matamshi yake aliyosema kwamba Rais wa zanzibar Dk Ali Mohaned shein ni dikteta na hatakaa madarakani na kufika mwaka 2020 viswani humu.

Post a Comment

0 Comments