Serikali ya Mapinduzi Zanzibar(SMZ ) imewaaagiza wakuu wa mikoa na
Wilaya kuwachukuliwa hatua za kisheria ikiwemo kuwasimamisha kazi
Watumishi wa Umma wanapuuzia maelekezobya serikalu na badalabyake
kuchukua mawazo ya baadhi ya viongozi wa Kisiasa wakati wa kutekelezw
majukumu yao.
SMZ A imesema haiwezekani kwa mtumishi wa Umma akaachwa aendelee
kupuuza na kusaliti maelekezo , maagizo au amri zinazotolewa na
serikali katika kuwatumikia wananchi huku wakiangalia macho vitendo vya
unyanyasaji na ubaguzi vikishamiri ilani watukishi hao wakikipwa
mshahara na Serikali inayotokana na jasho la wananchi.
Makamu wa Pili wa Rais Balozi Seif Ali Idd ametoa msimamo huo jana
wakati akizungumza na viongozi wa halmashauri za wikaya za CCM toka
Mikoa miwili ya Kusini na Kaskazini Pemba kikao kilichofanyika katika
kiwanda cha Makonyo na Rri ya Mafuta huko Wawi Mkoa wa Kusini Pemba.
Balozi Seif alisema taratibu za kuwafukuza watumishi waliosimamishwa
na watakaosimamishwa kazi kwa mujibu wa kanuni, taratibu na sheria za
utumishi Serikalini zitafuata hapo baadaye kwa wale watakaoshindwa
kubadilika kutokana na kushabikia siasa na kuacha majukumu yao ya ajira
Alieleza kuwa SMZ haiwezi kuvumilia maovu ya watu na hata mtu mmoja
atakayoyafanya dhidi ya Serikali huku kitolea mfano matendo ya kuwatenga
baadhi ya wananchi na kunyimwa kupatiwa huduma muhimu za kijamii kama
usafiri wa baharini, magari na kukataliwa kununua au kuuziwa bidhaa
"Kuanzia sasa Dc na Ma RC mkimbaini mtumishi wa serikali anasaliti na
kupuuza maagizo ya serikali msimakisheni kazi, taratibu na kanuni
zitafuata naadae"alisema Balizi seif
Alisema SMZ litahadharisha na kuwaeleza kuwa inaelewa kuwa hali ya
mitafaruku kisiwani Pemba ina kuwa kwa malengo maalum na wanasiasa
uchwara. Hivyo kupitia vyombo vya dola alisema italazimika kuimarisha
ulinzi ili kuwapa fursa wananchi waendelee kupata wasaa mpana wa kuishi
kwa amani, utulivu na upendo miongoni mwao.
Balozi Seif alisema cheche za shari na uvunjifu wa amani zinazojiri sasa
kisiwanibhuku zina dhamira ya wazi ya kutaka jamii ya kimataifa iione
Zanzibar kuna tatizo na vurugu zilizosababishwa na matokeo ya uchaguzi
wa mwezi wa oktoba ambao uliofutwa kisheria na Tume ya Uchaguzi
Zanzibar kwa mujibu wa sheria.
"Mfumo wa vyama vingi Barani Afrika ikiwemo Zanzibar una safari ndefu
kueleweka pengine hali hiibkwa Tanzania imethibitishwa na ripoti ya Jaji
Francis Nayalali ambapo wanqnchi asilimia 80 walipinga vyama vingi
na asilimia 20 kutataka mabadiliko ya mfumo wa kisiasa "alikumbusha.
Alisema kujenga chama cha siasa na kukubakika si janbo la kufumba macho
na kufumbua hivyo vyama vichanga huwaza kushika madaraka ya utawala na
kusahau kujiimarisha na kukubalika kama ilivyo CCM .
Akizungumzia wananchi waliopatwa na mitihani ya kufanyiwa hujuma mara na
baada ya uchaguzi mkuu Balozi Seif alisema Serikali Kuu inafikiria
kuangalia namna itakavyoweza kuwasidia wananchi waliohujumiwa mali zao,
vifaa na vyombo vyao vya usafiri.
Alisema nia njema ya seriiali za ccm kukubali kusikiliza hata maoni ya
wachache ilibkuruhusu vyama vingi inayoonekanq kutumiwa vibaya na
viongozi wasaka madaraka kwa hila ,nguvu na matumizi ya siasa za
ukabila na mgawanyiko.
Mapema Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa, Serikali za Mitaa
na Idara Maalum ya SMZ Haji Omar Kheir aliwahimiza wakuu wa wilaya na
mikoa kisiwani humu kutambua kuwa dhamana ya ulinzi wa amani na usalama
wa watu iko mikononi mwao hivyo wana wajibu wa kusimamia kila hatua .
Waziri Haji alisema usimamizi wao imara wa sera za serikali, maagizo na
tataribu za kiutawala na zile za kiutumishi sasa zinahitaji kusimamiwa
kwa weledi, umakini na vitendo kuliko wakati mwingine wowote.
"SMZ inajua na dunia ya wapenda amani inatambua kuwa kuna wanasiasa
wapenda madaraka ambao wameshindwa uchaguzi wanachochea ghasia na
kueneza sumu ya maneno ili amani, utukivu na uendo vitoweke pemba ili
wao wayafikie matlaba yao"alisema waziri huyo wa smz
Waziri Haji alisisitiza kuwa haipendezi kuona maamuzi mengine na masuala
madogo ambayo yako chini ya dhamana ya viongozi hao yakisubiri
kuamuliwa au kuchukuliwa hatua stahili na Rais au Makamu wa Pili wa
Rais wakati masuala mengine yao katika uwezo wao.
"Serikali imekupa dhamana ya kiutawala ili kutenda haki mahali stahili
lakini msishindwe kufanya maamuzi magumu ikiwa litajitokrza kundi la
watu wajaokusudia kuvuruga amani ya nchi na usalama wa watu. "Alisema
waziri huyo.
Makamu wa pili wa Rais na msafara wake yuko kisiwani Pemba iliwatembelea
wananchi kwa lengo la kuwafariji na kuwapa pole wale ambao mashamba yao
na wao wenyewe kudhuriwa na watu ambao hadi sasa hawajajulikana.
0 Comments
unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia