Ticker

6/recent/ticker-posts

HALMASHAURI YA JIJI LA ARUSHA MATATANI

 
Nembo mpya jiji la Arusha 
Halmashauri ya jiji la Arusha imeingia matatani mara baada ya kudaiwa kuipatia mkataba kampuni ya kuwasha taa za barabarani jijini hapa ya Skytell Ltd  ihali kampuni hiyo ilimaliza mkataba wake mwaka jana mwezi julai.

Mbali na kuipatia mkataba huo wa mwaka mmoja pia uongozi wa jiji hilo umedaiwa kuchukua fedha kiasi cha sh,5 milioni kama ada ya ushuru wa mabango kwa mwezi Agosti mwaka huu.

Kwa mujibu wa taarifa zilizolifikia gazeti hili zimedai kuwa uongozi wa jiji hilo uliipatia mkataba wa mwaka mmoja kampuni hiyo mnamo Agosti 8 mwaka huu.

Taarifa hizo zimeeleza kwamba katika mkataba huo nambari 0251 uliosainimwa na mhandisi mkuu wa jiji hilo,Afwilile Lamsy  uliitaka kampuni hiyo kulipa kiasi cha sh,70,444,800 milioni kuanzia mwezi julai 2013 hadi June 2014 kama ada ya mwaka mzima.

Hatahivyo,taarifa za uhakika zimedai kuwa  kampuni ya Skytel ilimaliza muda wake mnamo mwaka jana mwezi julai  na hadi sasa hakuna zabuni yoyote iliyofunguliwa ya kuwasha taa za barabarani jijini Arusha.

Vyanzo vya habari vimedai kwamba uongozi wa jiji la Arusha kwa sasa ndiyo unausimamia mradi wa taa za barabarani jijini hapa hadi pale zabuni za mradi huo zitakapofunguliwa.

Mkurugenzi wa kampuni hiyo,Allbles Shoo alipoulizwa kuhusiana na taarifa hizo mbali na kukiri kampuni yake kupatiwa mkataba  huo alisema kwamba alishatoa kiasi cha sh,5 milioni kama ada ya mwezi Agosti mwaka huu.

Hatahivyo,alipoiulizwa ya kuwa iweje apatiwe mkataba huo ihali muda wake ulimalizika mwaka jana alisisitiza kwamba yeye alifuatwa na watumishi wa jiji hilo ambao walimpatia mkataba na risitiza za malipo baada ya kuwalipa kiasi hicho.

Kaimu mkurugenzi wa jiji la Arusha ambaye pia ni mhandisi mkuu wa jiji hilo,Lamsy alipotafutwa alisema kuwa kulitokea makosa kwa wakala aliyeidhinishwa na jiji hilo kukusanya ushuru wa makampuni mbalimbali yanayofanywa kazi na jiji hilo.

Lamsy,alimtaja wakala wa Robert Advertisment kwamba ndiye aliyempelekea mkataba kampuni hiyo kimakosa na kudai kwamba suala hilo linashughulikiwa ndani ya vikao vyao hadi sasa.

Post a Comment

0 Comments