Ticker

6/recent/ticker-posts

AZANIA BANK WALIVYOSHIRIKI SAFARI MARATHON


Meneja wa Azania Bank tawi la Mbauda akimalizia hatua katika mbio za Safari marathon,mshiriki huyu ndiye pekee alikuwa mwenye umri mkubwa kwa upande wa changamoto za shirika .Alitumia dakika 40 kuhitimisha mbio zake na kuzawadiwa mapumziko ya siku mbili katika hotel ya New arusha hotel na waandaaji wa Safari marathon.
Afisa Masoko kanda ya kaskazini Bhoke Jackson akimalizia hatua za mwisho katika mbio za Safari marathon zilizo fanyika jijini Arusha.
Maafisa wa benki ya Azania walioibuka vinara dhidi ya wenzao katika mbio za kasi zaidi kwa jinsi ya kiume waliopo Benki ya Azania, kulia ni mshindi wa kwanza Mohamed Goagoa,mshindi wa pili Jumanne Lucawa na mwingine ni Afisa masoko tawi la Mbauda Salim Msangi.
Meneja wa Azania Bank tawi la Moshi Hajira Mmambe akimalizia kukimbia wakati wa mbio za Safari marathon zilizo fanyika jijini Arusha.
Wafanyakazi wa Benki ya Azania wakiwa katika picha ya pamoja nyuma ya banda lao.
Meneja wa matawi ya benki ya Azania kanda ya kaskazini,kutoka shoto ni Everist Mhogosi(meneja tawi laMbauda),Hajira Mmambe(meneja tawi la Moshi) na Leonird Maliwa meneja tawi la Arusha city.
Wafanyakazi wa Benki ya Azania wakijipongeza kwa msosi mara baada ya kuhitimishwa kwa mbio za Safari marathon zilizofanyika jijini Arusha.

Post a Comment

0 Comments