Ticker

6/recent/ticker-posts

KUMBE MAGAIDI WALIOLIPUA NAIROBI WALIPITIA JIJINI ARUSHA

  Shambulio hilo ni la pili kufanyika kwenye maeneo mawili tofauti ndani ya saa 24, baada ya lingine lililofanyika kwenye Mji wa Wajir, muda mfupi baada ya taarifa za kudhibitiwa kwa watu wanaodhaniwa kuwa magaidi walioshambulia jengo la kibiashara la Westgate mjini Nairobi.
Nairobi. Wakati Serikali ya Kenya imeliomba Shirika la Polisi la Kimataifa (Interpol) kumkamata Mwingereza Samantha Lewthwaite (pichani), taarifa zinadai kuwa mwanamke huyo alipitia mpaka wa Namanga, Arusha kwenda Nairobi ambako anahusishwa na tukio la ugaidi.Lewthwaite, ambaye ni maarufu kwa jina la ‘Mjane mweupe’ inaaminika anashirikiana na kundi la magaidi la Al-Shabab la SomalPicture
Nairobi. Wakati Serikali ya Kenya imeliomba Shirika la Polisi la Kimataifa (Interpol) kumkamata Mwingereza Samantha Lewthwaite (pichani), taarifa zinadai kuwa mwanamke huyo alipitia mpaka wa Namanga, Arusha kwenda Nairobi ambako anahusishwa na tukio la ugaidi.Lewthwaite, ambaye ni maarufu kwa jina la ‘Mjane mweupe’ inaaminika anashirikiana na kundi la magaidi la Al-Shabab la Somalia.
ia.
 
Kundi hilo ndilo linaaminika lilihusika na mashambulizi kwenye jengo la Westgate jijini Nairobi, wikiendi iliyopita.

Hata hivyo, taarifa ya Interpol ilisema kuwa alikuwa anatakiwa kujibu mashtaka ya kumiliki mabomu na kupanga njama za ugaidi Desemba 2011.
Interpol haikuhusisha maombi hayo ya Serikali ya Kenya na mashambulizi ya Nairobi.
Pia Lewthwaite inasemekana aliingia nchini humo kwa kutumia mpaka wa Tanzania.
Baadhi ya vyombo vya habari vya Afrika ya Kusini, vinasema mwanamke huyo alitumia pasi ya kusafiri ya nchi hiyo kuingia Kenya kwa kutumia mpaka wa Namanga uliopo mkoani Arusha.
Taarifa hizo zinasema mwanamke huyo alitumia mpaka wa Lunga Lunga na Namanga kati ya Februari na Agosti mwaka 2011 akitumia jina la Webb.
Habari hizo zinaeleza kuwa, awali mwanamke huyo alikuwa anaishi Afrika Kusini ambako aliweza kukopeshwa fedha benki na kuweza kupanga sehemu ya kuishi.
Wakati huohuo, watu wanaodhaniwa kuwa magaidi wamefanya shambulio kwenye Kituo cha Polisi mjini Mandera na kuua askari wawili, kujeruhi watatu kisha kuchoma zaidi ya magari 11 jana asubuhi.
Shambulio hilo ni la pili kufanyika kwenye maeneo mawili tofauti ndani ya saa 24, baada ya lingine lililofanyika kwenye Mji wa Wajir, muda mfupi baada ya taarifa za kudhibitiwa kwa watu wanaodhaniwa kuwa magaidi walioshambulia jengo la kibiashara la Westgate mjini Nairobi.
Shambulio hilo limefanyika wakati kikosi maalumu cha wataalamu wa mabaki ya mabomu wa Kenya na wale wa kimataifa kikianza kufanya upekuzi wa jengo hilo, ili kubaini wahusika halisi wa shambulio hilo na aina ya silaha zilizotumiwa.

Post a Comment

0 Comments