Ticker

6/recent/ticker-posts

TAASISI ZA SERIKALI ARUSHA ZASHINDWA KULIPA DENI LA MAJI LA ZAIDI YA MILIONI 322


Mamlaka ya Maji safi na maji taka mkoa wa Arusha(Auwsa)imeshindwa
kufikia malengo yake ya ukusanyaji wa mapato kwa asilimia 100 kutokana
na baadhi ya Taasisi za Serikali kushindwa kulipia ankra za maji zenye
thamani ya zaidi ya shilingi Milioni 322

Hayo yameelezwa na Mkurugenzi wa mamlaka hiyo mhandisi Ruth Koya
wakati akitoa taarifa kwa Naibu waziri wa Maji Binilith Mahenge mapema
jana Jijini hapa

Mhandisi Koya alisema kuwa taasisi hizo ni pamoja na Jeshi la Polisi
linalodaiwa kiasi cha shilingi Milioni 287 wakati Jeshi la wananchi
linadaiwa kiasi cha milioni 7.1 jambo ambalo limechangia kwa kiwango
kikubwa sana kufanya mamlaka hiyo kushindwa kufikia malengo yake

Pia alitaja Taasisi nyingine ambazo ni wadaiwa sugu wa mamalaka hiyo
ikilinganishwa kuwa ni taasisi za Serikali ni pamoja na Shule ya
Arusha(Arusha School)ambayo nayo inadaiwa kiasi cha Milioni 20 huku
nayo hospitali ya mkoa nayo ikidaiwa kiasi cha Milioni 26.

“tumejitaidi sana kuhakikisha kuwa tunafikia malengo yetu kwa asilimia
mia moja lakinim imeshindikana kwa kuwa hizi taasisi za serikali
zinatumwamisha hivyo basi tunaomba msisitizo wako Mheshimiwa waziri
kwani malengo yetu yakitimia basi wananchi wataweza kupata huduma
staili za maji”aliongeza mhandisi huyo.

Katika hatua nyingine mhandisi huyo alidai kuwa  mamalaka hiyo
imejipanga kukusanya kiasi cha shilingi billion 9.7 kwa kipindi cha
mwaka 2013 huku kwa mwezi wakiwa na malengo ya kukusanya zaidi ya
shilingi milini 400.

Katika hatua nyingine naibu waziri wa maji Binilith Mahenge alisema
kuwa kiwango hicho ambacho kinakusanyawa kwa mwezi  ni kidogo
hakitoshelezi ikilinganishwa kuwa jiji la arusha ni kubwa hivyo
jitihada za kuongeza mapat0 hayo zinahitajika .

Alitaja jitihada hizo kuwa ni npamoja na kuthibiti upotevu wa maji
ambao unafanywa na baadhi ya wateja wasio kuwa waaminifu hivyo
kusababisha mamlaka hayo kukosa mapato ya uhakika .

Mbali na hayo Naibu waziri huyo aliitaka mamlaka hiyo ihakikishe kuwa
inatekeleza mikakati iliyojiwekea ikiwemo kuongeza kiwango cha
uzalishaji wa maji kutoka elfu sitini na tano hadi kufikia lita elfu
tisini na tatu ili iweze kuwahudumia wananchi wote wa Jiji la Arusha

Alimalizia kwa kuwataka wafanyakazi wa mamalaka hiyo kuhakikisha kuwa
nao wanachangia mapato ya mamlaka hiyo kwa kudhibiti wizi na upotevu
wa maji kwani mamlaka hiyo ikiwa na mapato mazuri basi hata maslahi
yao nayo yatakuwa vizuri.

Post a Comment

0 Comments