KITITA cha
sh. milioni 100 kitatumika kugharamia shughuli ya mazishi na msiba wa
mfanyabiashara maarufu wa madini ya Tanzanite, aliyeuawa juzi kwa
kupigwa risasi na watu wasiojulikana.
Tajiri huyo Erasto Msuya
ambaye ni ambaye ni mtoto wa pili kati ya saba wa Elisaria Msuya maarufu
kwa jina la Kikaango alipigwa risasi zaidi ya kumi, na watu
wasiojulikana katika eneo la Mjohoroni, katikati ya mji wa Bomang’ombe
na Uwanja wa Kimataifa wa Kilimajaro (KIA), alipokuwa akisafiri kutoka
Moshi kwenda Arusha, juzi mchana.
Mmoja wa wajumbe wa kamati ya
mazishi aliyezungumza na theNkoromo Blog, kwa sharti la kutotajwa jina,
amesema kiasi hicho fedha kitaghramia kununua jeneza na kukodisha gari
maalum ya kubeba mwili kutoka jijini Arusha kwenda Mirarani, wilayani
Simnajiro ambako mazishi yamepangwa kufanyika Jumanne ijayo.
Amesema,
jeneza na gari la kubeba mwili tayari vimeagizwa jijini Nairobi, Kenya
kwa gharama ya sh. nane na kufafanua kwamba wamelazimika kukodisha gari
maalum ya kubeba maiti kutoka Nairobi kwa kuwa barabara ya kwenda
Mererani kuwa mbaya kiasi cha kuhitaji gari lenye uwezo mkubwa tofauti
yanayopatikana jijini Arusha ambayo mengi ni madogo.
Kamati ya
maandalizi ya mazishi hayo inaongozwa na Gady Msuya, kaka mkubwa
marehemu na leo wajumbe walikuwa wakikutana kwa vikao nyumbani kwa
mareehemu eneo la Kwa Idd, nje kidogo ya jiji la Arusha kukamilisha
mipango ya mazishi hayo huku waombolezaji wanaomiminika nyumbani kwa
marehemu wakikirimiwa kwa vyakula na vinywaji wahudumu wakiwa ni maalum
kutoka hotel ya SG Resort inayomilikiwa na marehemu Msuya.
Kifo
cha tajiri huyo, kimeacha utata miongoni mwa wafanyabiashara wenzake
ambao wengi wanaendelea kuhoji kwanini mwenzao ameuawa kwa kupigwa
risasi nyingi kiasi hicho na watu ambao hawakuondoka wala kupora mali
yoyote?
0 Comments
unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia