Ticker

6/recent/ticker-posts

MWENYEKITI WA KIJIJI ATUHUMIWA KWA KUUZA ARDHI YA KIJIJI KIHOLELA

MWENYEKITI wa kijiji cha Losirwa kata ya Esilalei wilayani Monduli bwana  George Arpakwa ametuhumiwa na wananchi wake kujihusisha na ufisadi wa uuzaji wa ardhi kiholela ya kijiji swala ambalo linakwamisha shughuli za kifugaji kijiji hapo.

 Wananchi wa kijiji hicho wakizungumza kwa masikitiko makubwa katika mkutano wa hadhara kijiji hapo wamedai kuwa wamechoshwa na uongozi wa mwenyekiti huo kushindwa kuonyesha uwadilifu wake kwa jamiii badala yake kuuza ardhi ya kijiji kinyume na sheria.

Mwenyekiti wa kijiji hicho ambae anatuhumiwa kujihusisha na kuuza ardhi ya kijiji baada ya kubaini kuwepo kwa waandishi wa habari eneo hilo  alichukua jukumu la kuvunja mkutano na kuleta vujo kwa baadhi ya viongozi wa kimila  akidai  kua waandishi wa habari hawaruhusiwi kuhudhuria mkutano huo huko akitokomea pasipo julikana.

Aidha Romeni ole Meiya akiwa mmoja wa kijiji hicho alisema kua alishangazwa sana kuona baadhi ya maeneo ya malisho ya mifugo na mapito ya mifugo sambamba na mabwawa kuwekewa uzio kuashiria kua mifugo hairuhusiwi kuingia eneo hilo licha ya maeneo hayo yakiwa yametengwa kwaajili ya mifugo.

Alisema hawana imani tena na mwenyekiti huyo   wa kijiji ambae sasa ameonyesha udhaifu wake katika utendaji wake wa kazi  hivyo wanamtaka achie ngazi na kwasasa hawamtambui kama yeye nikiongozi wa jamii hiyo ya kifugaji kwa kujihusisha na kuuza ardhi ya wafugaji kinuyme na sheria za kijiji husika.

Nae Kiteho  Richard alisema kunaashiria kijiji hicho kuwepo kwa ufisadi mkubwa  wa ardhi huku akihoji kwanini mwenyekiti alipobaini kuwepo kwa waandishi wa habari eneo hilo  kutokomea pasipojulikana huku akijua waandishi ni watu wa amani siku zote.

"Kama mwenyekiti hahusiki na kuuza maeneo ya wananchi kwanini amekimbia mkutano hii inaonyesha kua anahusika kwa asilimia kubwa ndio mana alipowaona waandishi wa habari akakimbia akijua siri  inafichuka" Alisema Richard"

Wananchi hao waliandamana hadi ofisi ya mwenyekiti huo nakuchukua jukumu kali lakutaka kuifunga ofisi hiyo wakiamini kua ninjia moja wapo ya kupata suluhisho la Ardhi yao kumilikiwa na wenye pesa wachache huku wakiomba serikali kushughulikia tatizo hilo likiwa bado halijaleta hadhari kubwa kwa jamii.

Kwa upande wake mkuu wa wilaya ya Monduli bwana Jowika Kasunga akizungumza kwa njia ya simu amekiri kupokea taarifa hizo za malalamiko ya wananchi nakuahidi kuwa anazifanyia kazi ilikubaini ukweli wa jambo hilo.

Post a Comment

0 Comments