Kikosi cha maswala ya ulinzi katika jumuiya ya
maendeleo ya nchi za kusini mwa Afrika(SADC) kimesema kuwa akitaendelea
kufungia macha mapigano yanayoendelea katika mji wa Goma uliopo
mashariki mwa nchini kongo .
Hayo yalibainishwa mkuu kikosi
cha secretariti ya ulinzi na mipango katika nchi za SADC kanali
Gerson Sangiza wakati akiongea na waandishi wa habari kuhusiana na namna
gani kikosi cha ulinzi kinasaidia mapigano ya nchini kongo.
Alisema
kuwa katika kipinchi cha nyuma walikuwa bado ya wapo katika mazungumzo
ya kujadili ni jinsi gani wanaweza kuisaidia nchi hii kongo kuondokana
na mapigano ambayo yameikumba nchi hiyo kwa muda mrefu .
Alisema
kuwa kwakua majeshi ya nchi za sadc yameundwa kwa ajili ya kuwasaidia
wananchi pamoja na kuwalinda hivyo wanajipanga vilivyo kwa ajili
kupeleka kikosi nchini kongo ya ili kuwasiadia wananchi wa nchini humo
ambao wameteseka kwa muda mrefu.
Pia alifafanua kuwa majeshi ya
nchi za sadc yameendelea kushirikiana kwa kipindi cha mda mrefu kwa
katika mambo mbalimbali ikiwemo viongozi wa nchi zetu kushirikiana kwa
kupeana ziara zakikazi,mafunzo ya kijeshi yakitolewa katika nchi yetu
ambapo alifafanua kuwa chuo cha kijeshi cha TMA kimekuwa kikichukuwa
wanafunzi kutoka nje ya nchi hususa ni nchi za sadc nawaleta kuwapa
elimu hapa nchini kwetu.
"pia tumekuwa tukitumia viongozi wetu
ambapo wamekuwa wanabadilishana ziara ambapo lengo kuu la ziara hizo ni
kubadilishana uzoefu pamoja na kujenga mahusiano"alisema Sangiza
Alisema
kuwa kazi nyingine ya majeshi haya ya sadc ni pamoja na kuwalinda
wananchi wa nchi hizi 15 na kuhakikisha kwamba kanda yetu hii
haitaingia tena katika
machafuko
Aliongeza kuwa majeshi haya yatasaidia pia wanachi
wasiweze kupata matatizo na pia kuhakikisha machafuko hayawezi kutokea
katika nchi hizi ili hali ya utulivu na amani iendelee kuwepo ili
maendeleo yawezekuwepo.
0 Comments
unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia