Ticker

6/recent/ticker-posts

SHIRIKA LA KISABATO LAFANIKIWA KUWASAIDIA MAALBINO ZAIDI YA 600

 Wadau wakisikiliza



Shirika la Kisabato la kusaidia majanga mbalimbali ya jamii (ADRA)mkoani hapa limefanikiwa kuwasaidia walemavu wa ngozi (ALBINO) zaidi ya 600 kutoka katika mikoa ya kanda ya kaskazini kwa kuwapa mahitaji muhimu kama vile elimu, Ajira, afya pamoja na usalama wao.

Akiongea na waandishi wa habari mapema jana katika Mkutano wa wadau mbalimbali wakiwemo viongozi wa watu wenye ulemavu wa Ngozi Askofu mkuu  wa kanisa la  Sabato ambaye pia ni raisi wa shirika hilo la kisabato Dkt Edwin Lwekundayo alisema kuwa hiyo ni moja ya mikakati ya kuhakikisha kuwa walemavu wanapata haki zao za msingi.

Dkt Edwin alisema kuwa shirika hilo limefanikiwa kuwapatia huduma za msingi walemavu kutoka katika Mikoa ya Arusha ,Kilimanjaro, pamoja na Tanga ambapo zoezi hilo limeanzia ngazi ya kata hali ambayo nayo imefanya matukio mbalimbali ya uuaji wa maalbino kupungua kwa kiasi kikubwa sana tofauti na hapo awali ambapo takwimu za mauaji zilikuwa kubwa sana.


Alifafanua kuwa huo ni mpango mkakati ambao pia ni mradi ambao ni endelevu na utaweza kufikia katika Mikoa yote ya Nchi ya Tanzania ambapo lengo halisi ni kuhakikisha kuwa maalbino wote wanakuwa katika hali ya usalama zaidi ingawaje kwa sasa mpango huo umedumu kwa miaka miwili ndani ya kanda ya kaskazini.

‘Lengo letu ni kuhakikisha kuwa maalbino wote wanakuwa katika mpango mzuri wa kimaisha na kupitia mradi huu tutaweza kuwafikia na kuhakikisha yale mahitaji ya msingi wanayapata kwani wengi wanakuwa katika hali ngumu ya maisha kwa kuwa  hawana muelekeo lakini sisi tunachokiitaji ni kuhakikisha kuwa wanasonga mbele zaidi nah ii itachangia sana hata kuweza kupunguza idadi ya vifo vya walemavu hawa’aliongeza dkt Edwin.

Awali mgeni rasmi katika ufunguzi wa  Mkutano huo George  Herbert ambaye ni  Naibu msajili wa mahakama ya biashara hapa nchini alisema kuwa kwa sasa kuna mkakati hasa kwenye Kesi za walemavu wa ngozi wa kuhakikisha kuwa zinamalizika  kwa wakati iili waweze kupata haki zao za msingi tofauti na pale ambapo kesi hizo zinaposhindwa kumalizika kwa wakati huku hali hiyo ikichangia sana Ongezeko la uonevu wa walemavu hao.


Herbet aliongeza kuwa pamoja na kuwa na mikakati hiyo ya kumaliza kesi za walemavu wa ngozi kwa wakati lakini bado Mahakama mbalimbali hapa nchini zinatambua na kuthamini haki za Albino hivyo nao wananchi wanatakiwa kuhakikisha kuwa  wanawafichua wale wote wanaosababisha madhara likiwemo suala zima la kifo kwa Maalbino.

Awali Meneja Mradi wa Shirika la Kisabato linalosaidia jamii kwenye masuala ya majanga,Bw Soulpeace Thomas Mzee alisema kuwa kupitia kwenye mkutano huo wa siku nne utasaidia sana kufikia  sera mkakati ambayo itaweza kuwasaidia walemavu wa Ngozi katika shuguli zao za kila siku kupitia kwenye chama cha Maalbino Tanzania,hali ambayo itaweza kuwapatia haki zao za ,msingi .

Post a Comment

0 Comments