Ticker

6/recent/ticker-posts

NMB YAOMBWA IKOPESHE NA WATEJA WA MAJUMBANI

 
WADAU mbalimbali wa benki ya NMB mkoani Arusha wameiomba benki hiyo kuanzisha  utaratibu wa kuwakopesha wateja wake nyumba za gharama nafuu ili kuwanufaisha  na  mikopo wanayokopa katika benki hiyo hususani wajasiriamali wenye kipato kidogo.

Pamoja na kuwa benki hiyo imekuwa ikitoa mikopo ya aina mbalimbali kwa wateja wake , hali hiyo imewawezesha kuwaondoa katika wimbi la umaskini  kwa kuanzisha miradi midogomidogo, ila kwa upande wa nyumba imekuwa ni changamoto kubwa kwao kwani bado benki hiyo haijaweza kuwasaidia .

Hayo yalielezwa na wafanyabiashara wananchama wa klabu ya NMB (NMB business club,)mkoani hapa,wakati walipohudhulia mafunzo ya  pili ya siku moja ya ujasiriamali yanayotolewa na benki hiyo kupitia virabu vya wajasiriamali vya NMB,ambapo mwaka huu yanayolenga kujua faida na athari za ushindani katika biashara  zao  yaliyofanyika  jijini hapa.

Alisema kuwa, asilimia kubwa ya wadau wa benki hiyo wamekuwa wakichukua mikopo kwa ajili ya kuboresha biashara zao ila wengi wao bado hawajaweza kujenga nyumba nzuri za kuishi hususani wenye vipato vya chini, hivyo endapo benki hiyo itaanzisha mchakato wa kuwajengea na kuwakopesha nyumba za bei nafuu wataweza kuwasaidia kuondokana na changamoto hiyo.

‘Kwa kweli benki hii imekuwa ikitusaidia  sana sisi  wajasiriamali  katika kuhakikisha tunajikwamua  na biashara na kuweza kuondokana na changamoto mbalimbali za kimaisha , hivyo endapo watatujengea nyumba hizo za bei nafuu tutaweza  kuishi maisha yaliyo bora zaidi’alisema Amina.
Aidha waliiomba benki hiyo ,kuanzisha huduma za viza kama wanavyofanya benki nyingine ili kuwawezesha kuchukua fedha hata  wawapo nje ya nchi ili kuweza kufanya bishara zao kwa uhakika zaidi wawapo nje ya nchi.

Akifungua mafunzo hayo , Meneja wa benki hiyo kanda ya kaskazini Vicky Bishubo  alisema kuwa benki hiyo imeboresha huduma  ya mikopo kwa wajasirimali kwa kiwango kikubwa kutoka shilingi milioni 1 na milioni 5 hadi kufikia sh, milioni 10 , hatua ambayo alisema itamsaidia mfanyabiashara mdogo kuongeza biashara zake na kujitanua zaidi.

Alisema kuwa , mafunzo hayo ambayo yamekuwa yakitolewa mwaka hadi mwaka yamekuwa yakiwawezesha wajasirimali hao kuboresha biashara zao  ikiwa ni pamoja na kubuni biashara mpya zenye tija ambazo zimewawezesha kujikwamua kiuchumi.

Bishubo alitaja malengo ya mafunzo hayo ni kuwawezesha washiriki kupata magfunzo ya msingi ya usimamizi wa biashara ,kuwawezesha washiriki kuelewa maana ya ujasirimali na kupata mbinu za kufanikisha biashara ba kuiendeleza ,pamoja na kuwawezesha kuwa na  ujasiri wa kuchukua mikopo.
 
Naye Mkuu wa kitengo cha wajasiriamali , Filbert Mponji alisema kuwa,benki hiyo imejiwekea mkakati ifikapo mwaka 2013 kuanzisha akaunti ya biashara kwa wajasirimali itakayowawezesha kuchukua fedha wakati wowote wanapohitaji.

Post a Comment

0 Comments