SEREKALI INAMPANGO GANI KUTEKETEZA MBOLEA FEKI :WARIDE JABU

MBUNGE wa Kiembe Samaki, Waride Bakari Jabu (CCM) ameihoji serikali ina utaratibu gani wa kuteketeza mbolea feki ambazo zimekuwa zikiingizwa nchini.
Waride alitoa kauli hiyo bungeni jana alipokuwa akiuliza swali katika kipindi cha maswali na majibu.
“Katika miaka ya hivi karibu mbolea feki isiyokidhi viwango imekuwa ikikamatwa kwenye maeneo mbalimbali nchini. Je, serikali ina mpango gani wa kuikusanya na kuiteketeza mbolea hiyo, ili kulinda afya za wananchi?” alihoji.
Akijibu swali hilo, Naibu Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Godfrey Zambi, alisema anakubaliana na mbunge huyo kuwepo kwa changamoto kwa pembejeo zisizokidhi viwango na ubora katika soko.
Alisema serikali kupitia sheria ya mbolea namba 9 ya mwaka 2009, ilianzisha Mamlaka ya Udhibiti wa Mbolea ili kuhakikisha mbolea inayotumiwa na wakulima nchini inakuwa kwenye ubora unaotakiwa kitaalamu.
Zambi alieleza mamlaka hiyo pamoja na mambo mengine, hufanya ukaguzi ili kuhakikisha kuwa mboleo ina ubora unaotakiwa.

Post a Comment

unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia

Previous Post Next Post