MIL. MOJA YATOLEWA NA KIDEFU KWA AJILI YA KUWAKAMATA WEZI WA LAMI


pichani ni mapipa ya lami yakiwa katika hali mbaya kutokana  kutotumika kwa miaka zaidi ya kumi sasa yakiwa nje ya ofisi ya mfuko wa maendeleo ya wananchi wa tarafa ya Kibosho, lami hiyo imekuwa ikibwa mara kwa mara kutokana na kutokuwapo na usimizi thabiti wa mali za mfuko huo.  
pichani ni mapipa ya lami yakiwa katika hali mbaya kutokana  kutotumika kwa miaka zaidi ya kumi sasa yakiwa nje ya ofisi ya mfuko wa maendeleo ya wananchi wa tarafa ya Kibosho, lami hiyo imekuwa ikibwa mara kwa mara kutokana na kutokuwapo na usimizi thabiti wa mali za mfuko huo.
Mwandishi wetu, Moshi

MFUKO  wa maendeleo wa wananchi wa Tarafa ya Kibosho wilaya ya Moshi Vijijini,umetoa ahadi ya zawadi ya pesa taslimu  shilingi Milioni moja kwa mtu atakayefanikisha kukamatwa kwa watu waliohusika na tukio la wizi wa lami mali ya mfuko huo.

Ahadi hiyo ilitolewa jana na mwenyekiti wa mfuko huo, Morris Makoi katika mkutano mkuu maalumu wa wanachama wa mfuko huo kufuatia wizi wa mapipa 35 uliofanywa na watu wasiojulikana Apili 17 mwaka huu.

Lami hiyo ambayo imedumu kwa maiaka 17 sasa,imekuwa haina uangalizi mzuri kutokana na kukosekana  kwa ulinzi wa uhakika na kutoa mwanya kwa wezi kuiba kiurahisi bila kukamatwa.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Moshi Vijijini, Morris makoi (kulia)akimgombeza dereva wa haice namba T686BYV (wa pili kushototo)bada ya dereva huyo kukutwa akosha gari lake pembezoni mwa barabara eneo la kibosho barabara ambayo imefanyiwa ukarabati hivi karibuni kwa kiwango cha moramu na halmashauri hiyo.
Akizungumza katika mkutano huo ambao hata hivyo uliahirishwa kutokana na kutofia idadi stahiki ya wajumbe,Makoi alisema kuwa,mtu yeyote mwenye taarifa sahihi juu ya nani aliiba lami hiyo na wapi imeuzwa,awasiliane na uongozi wa KIDEFU .

Mfuko huo wa maendeleo ya wananchi wa tarafa ya Kibosho ulianzishwa kwa lengo la kuharakisha maendeleo kwa wananchi ikiwamo ujenzi wa shule,hospital na kuboresha miundombinu ya barabara .

Katika kufanikisha mfuko huo,wananchi walikuwa wakikatwa shilingi mbili kwa kila kilo moja ya kahawa kwa ajli ya kutunisha mfuko huo na lami hiyo ilikuwa itumike kwa ajili ya ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami.

Hata hivyo mfuko huo uliyumba na kusambaratika na hivyo kushindwa kufikia malengo yaliyokusudiwa ambako kwa sasa wananchi wameamua kwa makusudi kuufufua mfuko huo.

Kwa mujibu wa mwenyekiti makoi ambaye pia ni diwani wa kata ya Okaoni na mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Moshi,wizi huo unatokea kutokana na kutokuwapo na usimamizi mzuri wa mali za mfuko huo kwa miaka kumi sasa..

Post a Comment

unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia

Previous Post Next Post