PSI KANDA YA KASKAZINI WATOA MAFUNZO KWA WAHUDUMU WA VITUO VYA AFYA VIPATAVYO 50 JIJINI ARUSHA

meneja mauzo wa PSI kanda ya kaskazini  Peleatian Masai akiwa anatoa mada kwa washiriki
 baadhi ya wahudumu wa vituo vya afya kutoka mikoa ya Arusha wakiwa wanafatilia kwa makini mafunzo yaliyokuwa yanatolewa na PSI katika ukumbi wa Olasiti garden  uliopo nje kidogo ya jiji
Mshauri wa huduma na bidhaa wa PSI Dr,Wambura Maseke akitoa mafunzo kwa washiriki katika hotel ya Olasiti


PSI Tanzania ni shirika lisilo la kiserikali linalotoa huduma za kiafya chini ya wizara ya afya na ustawi wa jamii, likimejikita katika idara za kinga za wizara hiyo.
 Katika kuhakikisha wakazi wa Arusha wanaendelea kupata huduma bora za afya  imetoa mafunzo kwa wahudumu wa vituo vya afya vipatavyo 50 vya serikali na vile vya watu binafsi ili kuboresha utoaji wa huduma bora za dawa za uzazi wa mpango zijulikazo kama (familia products and services) zinazosambazwa na shirika hilo.

Post a Comment

unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia

Previous Post Next Post