Ticker

6/recent/ticker-posts

MBUNGE AWAPATIA WANACHI SOKO LILILOFUGWA KWA MUDA WA MIAKA KUMI

Wananchi wa kata ya mbuguni wamempongeza mbunge wao wa jimbo la arumeru mashariki Joshua Nasari kwa kutimiza ahadi ya kurejesha soko la mbuguni lilisimamishwa kufanya kazi kwa muda wa miaka ipatayo 10 ikiwa ni kupisha  ujenzi wa stendi ya magari katika soko hilo .

Wanachi hao ambao ni wafanyabiashara wa soko hilo la Mbuguni wakati wakizungumza na Redio hii walisema kuwa  wanampongeza mbunge wao kwa kufikia hatua nzuri ya kurejesha soko hilo kwani wamekua katika wakati mgumu kwani walichukua mikopo ya biashara lakini toka mwaka 2003 akuna biashara waliofanya baada ya kusimamishwa kufanya biashara hiyo na kupisha ujenzi wa stendi ya mabasi .

Mmojawapo wa mfanyabiashara wa zamani kutoka katika soko hilo la Mbuguni  Bi Grace Kaaya alielezea kuwa ujio wa soko hilo umewasaidia sana ijapokuwa kwa sasa hivi wanakabiliwa na hali ngumu ya kutokuwa na mitaji ya kuanza biashara mpya.

“Unasikia ndugu mwandishi tunamshukuru sana mheshimiwa mbunge kwa kuwa wakati soko hili linafungwa tulikuwa tunauwezo wa kusomesha watoto wetu na sasa tukashindwa kwa hali hii tunatarajiwa tutaweza kuwalipia ada watoto wetu”, Alibainisha Bi Grace.

Pamoja na kuona kuwa ujio wa soko hilo unaleta nafuu pia alitoa rai kwa Halimashauri ya Wilaya ya Arumeru pamoja na Mbunge kuakikisha kuwa wanaboresha hali ya miundo mbinu ya soko hilo ili kuwawaezesha kufanya biashara zao kiufanisi zaidi.

Naye katibu wa  mbunge wa Arumeru Mashariki Bwana Totinani  Ndone alisema kuwa kwa mujibu wa sheria za serikali za mitaa amabapo inaeleza kuwa  Halimashauri  endapo inataka kufanya mswala ya Maendeleo  ni  shuruti  kuwajulisha wakazi husika na kukubaliana na sio kujichukulia uwamuzi pasipo kufikia makubaliano.

Ambapo alitoa rai kubwa kwa uongozi wa Halimashauri ya Wilaya ya Arumeru kuhakiksha kuwa wakazi wa Wilaya hiyo wanayo Moyo mkubwa wa kushirikiana nao hivyo ni budi kushirikiana nao kwa upana mkubwa ili kuiletea maendeleo katika halimashauri hiyo ya Arumeru.
Wakati huo huo  Mkurugenzi wa Wilaya Arumeru bwana Transes Kagenzi  alipozungumza na gazeti hili  alisema kuwa halimashauri yake imetenga jumla ya shilingi  milioni 50 kwa ajili ya ukarabati wa soko hilo sambamba na kuangalia jinsi gani ya kutatua miundo mbinu chakavu ya soko hilo ikiwemo tatizo la maji pamoja na huduma ya vyoo.

Post a Comment

0 Comments