Viongozi wa madhehebu mbali
mbali ya dini wametakiwa kudumisha umoja na mshikamano sanjari na kuacha
kudharaulina kwani hilo litaleta kumong’onyoka kwa maadili na kubomoa amani
yetu na badala yake kuhubiri ushirikiano na kuwajenga waumini wao kuwa na hofu
ya mungu.
Kauli hiyo imetolewa na
Katibu mkuu wa ccm ndugu Abdurahaman Kinana kwenye maadhimisho ya siku ya kumbu
kumbu imamu Husein yanayoadhimishwa na dhehebu la khoja Ithnasher kote duniani
na kufanyika kwenye msikiti wa jamii hiyo jijini hapa juzi.
Kinana alisema kuwa hivi
sasa jamii ya watanzania imeingia kwa baadhi ya watanzania kuwauza wenzao huku
ni kutaka kuleta mpasuko kiimani na wengine kujenga uadui kwa kudharau
madhehebu za wenzao tufike mahali tuheshimu na kujifunza yale yalio kwa
mwenzako kwa ustaarabu na kuvumiliana.
“Ustaarabu wa kuvumiliana
na kuweka upendo miongoni mwetu ndiyo silaha ya kuitunza amani iliyopo hapa
nchini nawaombeni viongozi wa dini hapa nchini kuwajenga waumini kuwa na hofu
ya Mungu ili taifa letu lisikumbwe na mipasuko ya kiimani”alisema Kinana
Akizungumza kwa niaba ya
mkuu wa mkoa huo Mkuu wa wilaya ya Monduli Jowika Kasunga alisema kuwa kumekuwa
na vikundi vya kiimani ambavyo vimesajiliwa lakini vimekuwa vikichochea
uvunjifu wa amani na kuvitaka kuacha kuipoteza amani iliyopo kwani kutafuta ni
gharama kuliko kuitunza
Kasunga alisema kuwa
anatoa wito kwa viongozi wa madhebu hapa nchini kuwajengea hofu ya Mungu watumishi
wa serekali na wananchi ilituishi salama kwa amani iliyopo serekali pekee
haiwezi kuitunza bila ya kushirikiana nanyi na watanzania.
Nae Sheikh wa mkoa wa
Arusha Shaban bin Simba alisema kuwa nchi kuingia kwenye machafuko ni jamii
kumuasi muumba wao na kutokuwa na hofu ya siku ya malipo na kuwataka viongozi
wa dini kujenga ushirikiano wa karibu na maskizano