Ticker

6/recent/ticker-posts

TRA YAANZISHA MFUMO WA KUTOA STEMPU KAZI ZA WASANII


Mamlaka ya Mapato nchini imeanzisha mfumo wa kutoa stempu kwa kazi za wasanii ili kudhibiti unyonywaji wa kazi  hizo unaofanywa na baadhi ya wasambazaji na wazalishaji feki hivyo kuwafanya wasanii wanufaike na kazi zao pamoja na kulipa kodi kwa serikali.

Akizungumza na Wasanii wa muziki na filamu jijini Arusha ,Afisa elimu kwa mlipakodi TRA,Frank Mwaselela amesema kuwa mfumo huo tayari umerasimishwa kisheria na baada ya kutoa elimu kwa wasambazaji na wasanii hakuna kazi yeyote itakayoruhusiwa kuuzwa pasipo kuwa na stempu.
Afisa huyo amesema kuwa mfumo huo utawasaidia wasanii kutoibiwa kazi zao  na pia kazi zao kuwa na ulinzio wa kisheria baada ya kupitia taratibu sahihi ambazo ni kuzisajili baraza la sanaa (BASATA) Na pia kwa baraza linalohusika na haki miliki (COSOTA).
Naye Afisa  Kodi  Msafiri Mbibo kutoka makao makuu ya TRA amesema kuwa mfumo huo wa stempu umeanza mwaka jana   utasaidia kuondoa wimbi kubwa la wizi na uharibifu wa kazi za sanaa .
“Mpango huu utasaidia kuhakikisha kuwa wasanii kuwa mikataba inayozingatia  haki za wasanii,tayari tuimeshaanza kufanya operesheni kuwakamata wanaouza kazi zisizo na stempu na kuharibu mashione mkoa wa Dar tutaelekea mikoani pia” Alisema Afisa huyo
Katibu wa Chama cha Wauzaji wa kazi za wasanii jijini hapa James Male amesema kuwa jitahada zinazofanywa na TRA na Serikali ni nzuri na ameiomba mamlaka hiyo kuzitazama kazi walizonunua miaka ya nyuma kabla ya kuanzishwa kwa mfumo wa stempu.
Mwenyekiti wa Chama cha Wasanii mkoani Arusha ,Kassim Digega ameipongeza mamlaka hiyo kwa kuonyesha nia ya dhati ya kulinda kazi zao ili waweze kunufaika na kulinufaisha taifa kwa kulipa kodi.

Post a Comment

0 Comments