BONDIA ALIBABA RAMADHAN WA KILIMANJARO ALIVYOMTWANGA ROY MBUNDA WA RUVUMA
| Kikundi cha ngoma kikitoa Burudani kabla ya pambano la Ngumi kuanza kati ya Bondia Alibaba Ramadhan wa Kilimanjaro na Roy Mbunda wa Ruvuma. |
| Mgeni rasmi katika pambano hilo mkuu wa polisi wa wilaya OCD Deusdedit Kasindo akizungumza kabla ya kuanza kwa pambano la ngumi katika ya bondia Alibba na Roy Mbunda. |
| Mwakilishi wa kampuni ya Panone ,Gido Marandu akizungumza kabla ya pambano hilo. |
| Mkurugenzi wa kampuni ya Ibraline ,Ibrahim Shayo akizungumza kabla ya pambano hilo. |
| Mmoja wa mabondia waliopambana katika mapambano ya utangulizi akitokwa mchuzi baada ya kuchezea masumbwi toka kwa Bondia Mwakipesile. |
| Bondia Mwakipesile(Shoto) akisukuma konde . |
| Hatimaye bondia Mwakipesile akaibuka mshindi kwa pointi |
| Likafuata pambano la Bondia Massawe toka kibosho . |
| Akapambana na Bondia Rasta toka jijini Arusha. |
| Bondia Rasta akachezea ngumi za kutosha toka kwa Mkibosho.Masawe. |
| Bondia Rasta akaomba Poooo.akasalimu amri akasema siendelei na pambano taumia. |
| Bondia Masawe toka Kibosho akapewa Ushindi kwa kumtwanga KO Bondia Rasta. |
| Likafuatia pambano kali tena na hapa ni kati ya Fredy George kutoka Himo mwenye Bukta ya njano na Pascaly Bruno wa Moshi. |
| Ngumi zikapigwa kwa raund zote nne. |
| Mabondia wote wakiwa hoi kama anavyoonekana Fredy George akivuliwa Groves. |
| Bondia Pascaly Bruno akatangazwa mshindi . |
| Baadae sasa likafuata pambano lililokuwa likisubiriwa na wengi ni la kuwania mkanda wa taifa kati ya Bondia Alibaba Ramadhan na Roy Mbunda. |
| Bondia Alibaba Ramadhan akiingia ukumbini akiwa anasindikizwa na wapambe wake. |
| Bondia Alibaba akipasha misuli moto kabla ya kuanza kwa pambano. |
| Pambano likaanza ndani ya round ya pili tu Bondia Alibaba anasukuma konde kwa bondia Roy Mbunda lililompeleka chini. |
| Baadae Roy Mbunda akaamka akigugumia maumivu ya mguu akidai msuli wa paja umebana. |
| Mwamuzi wa pambano hilo Said Chaku akalazimika kutaka kufahamu endapo Mbunda ataendelea ama la. |
| Mwamuzi Chaku akalazimika kukatisha pambano kutokana na Bondia Mbunda kuda hatoweza endelea na pambano. |
| Roy Mbunda akisikilizia maumivu. |
0 Comments:
Post a Comment
unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia