Ticker

6/recent/ticker-posts

KINANA AWAOMBA RADHI WANANCHI WA KAREMA


 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwahutubia wakazi wa Kapalamsenga wilayani Mpanda mkoani Katavi.
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akiwahutubia wakazi wa Kapalamsenga ambapo aliwaambia wananchi hao kuwa CCM inazidi kuimarika na kuzidi kuaminika kwa wananchi siku hadi siku .


 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungmza mbele ya waandishi wa habari kwenye eneo lililopaswa kujengwa bandari ya Karema baada ya kujionea mradi wa ujenzi wa bandari ya Karema ulivyosimama.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiangalia majengo yaliyokuwa yameenza kujengwa kisha mradi wa ujenzi wa bandari kusimama kwa muda mrefu,Katibu Mkuu yupo kwenye ziara ya siku tatu mkoani Katavi ambapo moja ya shughuli atakazofanya ni kukagua utekelezaji wa ilani ya uchaguzi na kujenga na kuimarisha Chama.

 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana ,akiongozana na Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye , Mkuu wa Mkoa wa Katavi Dk. Rajab Rutengwe wakikagua mradi wa Ujenzi wa Mwalo uliopo kijiji cha Ikola.


  • Awaomba radhi wananchi wa Karema kwa kuchelewa kukamilika kwa mradi wa bandari ambao umesimama kabisa baada ya mkandarasi aliyepewa mradi huo kushindwa kuumaliza .
  • Asikitishwa na watumishi wengi wa serikali kuendeleza tabia ya umangi meza kwani miradi mingine inasimama kwa kipindi kirefu kwa sababu kuna kiongozi wa serikali amechelewa kujibu barua itakayofanikisha mradi kuendelea na kumalizika kwa wakati.
  • Asisitiza Viongozi na wana CCM kuwa wakali katika kusimamia utekelezaji wa ilani ya uchaguzi na kusema si vyema tusubiri wapinzani waseme ,tunayaona matatizo inabidi wana CCM wayasemee wenyewe na si vinginevyo.

Post a Comment

0 Comments