BREAKING NEWS

Thursday, April 3, 2014

MeTL YASHINDA TUZO 3 ZA RAIS ZA WATENGENEZAJI BIDHAA KWA MWAKA 2013

DSC_0716
Na. Mwandishi wetu.
Makampuni matatu makubwa yaliyo ndani ya MeTL Group hivi majuzi yamefanikiwa kutwaa tuzo za Rais za Watengenezaji Bidhaa kwa mwaka 2013.
Makampuni hayo ni: East Coast Oils & Fats Ltd ya Kurasini ambayo hutengeneza sabuni na mafuta ya kupikia pamoja na bidhaa nyingine.
Afritex Limited ambayo hutengeneza Khanga, Vitenge na bidhaa zifananazo; na 21st Century Textiles ambayo ni kampuni kubwa na ya kisasa Afrika Mashariki na kati inayotengeneza bidhaa kama khanga, vitenge, vikoi, mashuka, nguo za kimasai n.k.
Tuzo ya Rais ya Watengenezaji wa Bidhaa ni tuzo ambayo hutolewa kwa makampuni mbali mbali nchini Tanzania yanayojihusisha na utengenezwaji wa bidhaa. Ubora wa bidhaa ndio hufanya kampuni kushinda tuzo hiyo.
DSC_0722 DSC_0723 DSC_0724

Share this:

Post a Comment

unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia

 
Back To Top
Copyright © 2014 MOUNT KILI NEWS. Designed by OddThemes | Distributed By Gooyaabi Templates