Ticker

6/recent/ticker-posts

CHIPUKIZI CUP KUTIMUA VUMBI DESEMBA 7 MWAKA HUU JIJINI ARUSHA





TIMU  mbalimbali kutoka nchi za Kenya,Uganda na wenyeji Tanzania zinatarajia kushiriki michuano ya Chipukizi Cup inayotarajia kutimua vumbi kuanzia desemba 7 hadi 9 mwaka huu katika viwanja mbalimbali mkoani Arusha.

Michuano hiyo imeandaliwa na taasisi ya  kukuza vipaji vya soka nchini ya Future Stars Academy ambapo ina lengo la kukuza sekta ya utalii nchini,kufahamiana,kukuza vipaji vya soka hususani kwa watoto wadogo.

Kwa mujibu wa mkurugenzi na mwanzilishi wa taasisi hiyo,Alfred Itaeli  alisema kwamba michuano hiyo itashirikisha timu za wavulana walio chini ya umri wa miaka U-10,U-12,U-14 na U-17 huku timu za  wasichana zikiwa chini ya umri wa miaka U-14 na U-17.

Itaeli,alisema kwamba michuano hiyo itapigwa katika viwanja tofauti ambapo ni uwanja wa Sheikh Amri Abeid,uwanja wa shule ya kimataifa ya Moshi sanjari na viwanja mbalimbali vilivyopo mkoani Arusha.

Alizitaka timu shiriki ikiwa ni pamoja na timu ya Alliance ya jijini Mwanza kuthibitisha ushiriki wao mapema huku akiitaja  ada ya usajili  kuwa ni $ 40 kwa kila timu shiriki ambapo alisisitiza kuwa kutakuwa na zawadi ya vikombe na medali kwa washindi wa timu mbalimbali.

Post a Comment

0 Comments