MAELFU YA WATU WAKUSANYIKA SHEIKH AMRI ABEID KUIOMBEA NCHI YETU


Alisema kuwa lengo ya kongamano hilo ni kuweka  agano la uzima na uhai  ili watu waweze kufurahia maisha na kuondokana na mizigo ya madeni na magonjwa mbalimbali.

Aidha alifafanua kuwa mbali na kuvunja maagano pia wananchi hao wa madhehebu mbalimbali wamepata fursa ya kuiombea nchi iwe na amani ikiwa ni pamoja na uchumi wan chi kukua ili wananchi waweze kupata maendeleo.

MAELFU  ya  wakazi wa jiji la Arusha  walikusanyika katika kongamano lililofanyika katika viwanja vya kumbukumbu wa sheikh amri Abeid ili kuvunja maagano pamoja na kuiombea nchi ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania ili iweze kuondokana na madeni.
Akizungumza katika viwanja hivyo Mtumishi wa Mungu Christian Mwabukusi alesema kuwa mfululizo wa maombi hayo ni kuvunja maagano mbalimbali ili kuweza kumuomba Mungu ili aweze kulinusuru taifa haswa katika madeni ya kurithi.
Bw.Mwabukusi alisema kuwa inabidi yafanyike maombi ya kuvunja maagano ili kuweka maagano mapya katika ulimwengu wa roho  ili Mungu aweze kusamehe na hatimaye nchi iweze kuwa na neema na  kuondokana na madeni.
Alisema kuwa lengo ya kongamano hilo ni kuweka  agano la uzima na uhai  ili watu waweze kufurahia maisha na kuondokana na mizigo ya madeni na magonjwa mbalimbali.
“Unajua kuna vitu vinafanyika katika ulimwengu war oho mfano kama rais wa kwanza aliondoka akaacha madeni utakuta rais atakeyekingia madarakani naye pia anaridhi madeni hatimaye taifa pia linaingia katika mrundikano wa madeni hivyo katika ulimwengu wa roho ni lazima maombi hayo yawezekufanyika ili kuvunja maagano na roho za  madeni”alisema bw.Mwabukusiha
Aidha alifafanua kuwa mbali na kuvunja maagano pia wananchi hao wa madhehebu mbalimbali wamepata fursa ya kuiombea nchi iwe na amani ikiwa ni pamoja na uchumi wan chi kukua ili wananchi waweze kupata maendeleo.
Alisema kuwa faida ya kuvunja agano ni kupata uzima ambapo pia mtu anaweza kuishi maisha kwa raha na kuondokana na mizigo ikiwa ni kudumu katika amani ambamo ndani yake kuna maendeleo ya kiuchumi,kijamii na maendeleo ya kimwili ili kuondokana na magonjwa mbalimbali.

Maombi hayo yameshirikisha maelfu wa wakazi wa Jiji la Arusha,Mwanza,Tanga,Dar es Salaam,Manyara na Kilimanjaro ambapo yameandaliwa na kituo cha radio na maombi cha Safina kilichopo katika Kata ya Kaloleni jijini Arusha.

Habari na mdau wa libeneke Ashura Mohamed,Arusha

About Woinde Shizza

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 Comments:

Post a Comment

unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia