TRA TATAKIWA KUFUNGUA OFISI MANYARA

Nembo ya TRA

MAMLAKA ya Mapato nchini (TRA) Mkoa wa Manyara imetakiwa kufungua ofisi yake Mji mdogo wa Mirerani Wilaya ya Simanjiro ili kuwawezesha madereva wa pikipiki za kubebea abiria (bodaboda) kukata leseni zao.


Hayo yameelezwa  na Mkuu mpya wa kituo cha polisi Mirerani,Mrakibu msaidizi wa polisi Mohamed Mkalipa wakati akizungumza na madereva wa pikipiki wanaotoa huduma ya usafiri wa abiria kwenye mji huo. 


Mkalipa alisema kutokana na umbali wa ofisi za TRA ulipo kati ya Babati na Mirerani unawafanya madereva wengi kushindwa kukata leseni,hivyo ni vema mamlaka hiyo ikaanzisha ofisi zao Mirerani ili madereva wapate huduma hiyo.


“Kutokuwepo ofisi za TRA wilaya hapa na pia kwenye mji mdogo wa Mirerani kunakwamisha kwa kiasi kikubwa upatikanaji wa leseni za madereva hivyo viongozi wa mamlaka hiyo wanapaswa walibebe kwa uzito,” alisema Mkalipa.

Pia aliwataka madereva hao kutii sheria za usalama barabarani na kutoa ushirikiano kwa askari wa usalama barabarani kupitia dhana ya polisi jamii kuliko kukimbia kila wakati wanapokuwa na makosa ya barabarani.

Alisema madereva wa pikipiki wanatakiwa kutii sheria bila shuruti kwa kutimiza masharti yote ya usafirishaji wa abiria ikiwemo kuvaa kofia ngumu wanapoendesha pikipiki kwa ajili ya usalama wao endapo wakipata ajali.


Hata hivyo,waendesha pikipiki hao waliunga mkono tamko la mkuu huyo la TRA kufungua ofisi zao kwenye mji huo kuliko kufika mara chache na kuwavizia kipindi ambacho hawana fedha za kulipia leseni.


“Kitendo cha TRA kutokuwa na ofisi za kudumu kwenye wilaya hii kinatukwaza sana,kwani sisi wenyewe tungekuwa tunakwenda peke yetu na kulipa fedha siyo kama sasa wanapokuja mara moja moja kwa kutuvizia,” walisema.

About Woinde Shizza

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 Comments:

Post a Comment

unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia