WAKILI WA RYANDIKAYO APEWA HADI JUNI 15, KUJIBU MAOMBI YA MWENDESHA MASHITAKA
Mahakama ya Kimataifa ya Mauaji ya Kimbari ya Rwanda (ICTR) imetoa hadi
Juni 15, mwaka huu kwa wakili wa zamu wa mtuhumiwa wa mauaji ya kimbari
ambaye bado anasakwa, Charles Ryandikayo kujibu maombi ya mwendesha
mashitaka ya kutaka kuihamishia kesi hiyo kwenda kusikilizwa nchini
Rwanda.
‘’Mahakama
inamwamuru wakili wa zamu kujibu maombi ya mwendesha mashitaka ifikapo
Juni 15, 2012,’’ inaeleza sehemu ya uamuzi huo wauliotolewa Mei 24,
2012.
Mwendesha
mashitaka Mei 9, mwaka huu aliwasilisha maombi mahakamani hapo ya
kutaka kuihamishia nchini Rwanda, kesi ya Ryandikayo, meneja wa zamani
wa mgahawa mmoja katika wilaya ya Gishyita pamoja na kesi nyingine
inayomkabili aliyekuwa Meya wa wilaya Gisovu, Aloys Ndimbati. Wilaya
zote zipo katika mkoa wa Kibuye.
Katika
maombi yake,wakili wa zamu wa mtuhumiwa Ryandikayo, Nelson Merinyo wa
Tanzania,aliomba muda wa wa miezi mitano ili kujibu hoja za mwendesha
mashitaka na kwamba alipokea nakala ya maombi hayo Mei 18, 2012.
Alifafanua kuwa anataka kujibu hoja hizo kwa ‘’ upana na kwa kina’’ hivyo kuhitaji muda zaidi kutimiza adhama hiyo.
Ryandikayo
anashitakiwa kwa mauaji ya kimbari, kula njama za kufanya mauaji hayo,
uhalifu dhidi ya binadamu na uhalifu wa kivita kwa ushiriki wao katika
mauaji ya kimbari ya 1994.
Kwa
mujibu wa hati hiyo ya mashitaka Ryandikayo alishiriki katika mauaji ya
maelfu ya wanaume, wanawake na watoto waliokusanyika ndani ya kanisa la
Mubuga na kuwaelekeza wanamgambo na polisi kulishambulia kanisa hilo
kwa risasi, mabomu ya mkono na silaha nyingine.
Maombi
hayo yamekuja baada ya maamuzi ya Mahakama Mei 8, 2012 kuhamishia
nchini Rwanda, kesi ya mtuhumiwa ambaye bado anatafutwa, Ladislas
Ntaganzwa.
Maombi
mengine matatu ya aina hiyo yameshatolewa uamuzi na ICTR ambayo
yanawahusu, Mchungaji Jean Uwinkindi na watuhumiwa wawili ambao nao bado
wanasakwa ikiwa ni pamoja na Fulgence Kayishema na Charles Sikubwabo.
Uamuzi
mwingine bado unasubiriwa juu ya mshitakiwa Bernard Munyagishari
anayesadikiwa kuwa kiongozi wa wanamgambo wa Interahamwe mkoani Gisenyi,
Kaskazini ya Rwanda.
0 Comments:
Post a Comment
unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia