WASICHANA WA JAMII YA KIFUGAJI WATAKIWA KUSOMA MASOMO YA SAYANSI

 wanafunzi wa jamii ya kimasai waisikiliza mada kwa makini
Wasichana wa jamii ya kifugaji wilayni Monduli mkoani Arusha,wametakiwa kupenda kusoma masomo ya sayansi iliyaweze kunufaika na teknolojia ya mbali mbali na kuisaidia jamii yao.

Meneja wa kanda ya kaskazini wa mamlaka ya mawasiliano(TCRA)Annete Matindi alitoa wito huo katika seminwa ya maadhimisho ya wiki ya mawasiliano simu na habari jamii katika shule ya sekondari ya wasichana ya Kipok wilayani Monduli.

Alisema wakati mamlaka hiyo ikiwa imejipanga kufikisha huduma za teknolojia ya mawasiliano hadi vijijini wasichana wa jamii ya wafugaji wanafursa kubwa ya kunufaika na huduma hizo.

“Huduma za mawasiliano sasa zinafika vijijini hivyo,kuna fursa kwenu kuzitumia katika kukabiliana na changamoto zinazowakabili”alisema Matindi

Matindi alisema TCRA imejipanga kuhakikisha huduma ya mawasiliano ya Intaneti inawafikia wananchi wengi ambao wanaishi vijijini ili waweze kuitumia kujifunza mambo mbali mbali kikiwemo kilomo cha kisasa na utaalamu wake.

Awali mkuu wa wilaya ya Monduli Jowika Kasunga alitowa wito kwa wasichana wa jamii hiyo ya kifugaji kujikita kusoma masomo ya sayansi katika kuipelekea jamii teknolojia mbali mbali watakazo kuwa wamejifunza

About Woinde Shizza

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 Comments:

Post a Comment

unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia