Ticker

6/recent/ticker-posts

SHIRIKA LA COMPASION LAZINDUA MIRADI MIKUBWA YA MAJI MKOANI ARUSHA

SHIRIKA la kidini linaloshughulika na watoto la Compasion hapa nchini limezindua miradi mikubwa ya maji yenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 600 katika vituo 7 katika jijini  Arusha, itakayo wanufaisha wananchi zaidi ya 200,000 waliokuwa wakikabiliwa na changamoto ya ukosefu wa maji safi ya kunywa.

Uzinduzi huo ulifanywa na kaimu katibu tawala wa wilaya ya Arusha,Yacobo Shayo kwa niaba ya mkuu wa mkoa wa Arusha,Magessa Mulongo mwishoni mwa wiki katika maeneo tofauti ya Olmatejoo,Kambi ya Fisi  na Unga limited jijini hapa.

Kwa mujibu wa mkurugenzi wa nchi wa shirika hilo la compassion nchini,Joseph Mayalla alisema kuwa uzinduzi huo ni mwendelezo wa mkakati wa shirika hilo katika kuwasogezea huduma mbalimbali wananchi ,ambapo katika mikoa 12 linayohudumiwa na Compasion hapa nchini  mikoa miwili ya Morogoro na Singida imenufaika na  mpango wa uzinduzi wa miradi ya Maji.

Alisema kuwa shirika hilo limefanikiwa kuzindua miradi hiyo kwa kushirikiana na washirika wake ambao ni makanisa  mbalimbali ya kipentekoste ya jijini hapa,na kwamba miradi hiyo itakuwa chini ya vituo vya kulelea  watoto  wasio na uwezo vilivyo chini ya makanisa hayo .

Alifafanua kuwa miradi hiyo imezinduliwa katika vituo vya,Pefa katika kanisa la Pentekoste lililopo Olmatejoo, kanisa la Jerusalem Baptist lililopo kambi ya fisi,kanisa la P.AG na kanisa la Free Pentecostal(FPCT)yaliyopo eneo la Unga limited na kanisa la Elim pentecoste lililopo kata ya daraja mbili.

Alisema kuwa katika miradi hiyo kituo cha kanisa la Free Pentecost  Unga Limited ,kulizinduliwa miradi mitatu ikiwemo jengo la watoto lenye  gorofa tatu litakalotumika  kama shule ya kufundishia watoto wanaolelewa kwenye vituo hivyo,ofisi pamoja na huduma zingine,kituo cha maji na Jenereta kubwa la umeme vyote kwa pamoja vimegharimu zaidi ya sh,milioni 200.

Mayala aliongeza kuwa shirika lake litaendelea kutoa huduma kwan jamii kupitia makanisa katika kuibua miradi na kuisogeza kwa wananchi na kwamba litaendelea kujikita zaidi kwenye miundo mbinu,Maji,usafi na Afya.
Alisema shirika hilo ambalo lilianza kutoa huduma hapa nchini mwaka 1999, kwa sasa linahudumia watoto zaidi ya 65,900 hapa nchini katika mikoa 12 linayoihudumia  na matarajio ni kuifikia mikoa yote hapa nchini.

Akizungumza baada ya uzinduzi huo mgeni rasimu katika miradi hiyo,Yacob Shayo alitoa wito kwa makanisa hayo kutochoka kutoa huduma kwa jamii kwani yamekuwa na mchango mkubwa sana  katika kudumisha amani na malezi  bora ya makuzi ya watoto.

Shayo aliwataka wananchi kuitunza miradi hiyo ili iweze kudumu na kuvinufaisha pia vizazi vijavyo ,wawe tayari kujitolea na kutoa wito kwa watu wasio taka maendeleo ama kufanya kazi waadhibiwe kwa kuchapwa viboko.

Post a Comment

0 Comments