SUPER SPORT YAITANGAZA TANZANIA KIMATAIFA KATIKA MEDANI YA MICHEZO KWA KUZINDUA WIKI YA SOKA TANZANIA

 Meneja Mkuu wa Multichoice Tanzania  Bw. Peter Fauel akifafanua ujio wa Super Sport nchini Tanzania na kuipongeza TFF kwa kuonyesha ushirikiano na kuwa Chaneli hiyo itaonyesha mechi tano za Ligi ya Tanzania kuanzia leo Ijumaa Septemba 28 hadi Jumatano Oktoba 3 mwaka 2012
 Rais wa Shirikisho la Mpira wa miguu nchini (TFF) Bw. Leordiga Tenga akitoa nasaha zake wakati wa uzinduzi wa wiki ya Soka Tanzania ambapo amevitaka vilabu vitakavyopata bahati ya kuonekana katika chaneli hiyo kuonyesha kiwango cha soka la Tanzania na kuzingatia nidhamu haswa mechi ya Watani wa Jadi Yanga na Simba ambao wanatambulika barani Afrika kama timu zenye upinzani mkali.
 Mkuu wa Super Sport barani Afrika Bw. Andre Venter akielezea furaha yake kuja Tanzania na kupata fursa ya kulitangaza soka la Tanzania kimataifa kupitia chaneli ya Super Sport amesema chaneli hiyo imechafanya kazi katika nchi za Kenya na Uganda na Sasa ni wakati wa Tanzania kuonyesha kiwango chake cha soka Kimataifa.

 Baadhi ya Wadau wa michezo wakipata viburidisho wakati wa uzinduzi wa wiki ya soka Tanzania
 Meneja Uhusiano wa Multichoice Tanzania Barbara Kambogi akitoa ufafanuzi kwa waandishi wa habari waliohudhuria uzinduzi huo kuwa Super Sport wakishirikiana na TFF wapo hapa nchini na kwa mara ya kwanza wanaonyesha mechi za Ligi ikiwemo timu ambazo hata siku moja hazijawahi kuonekana kwenye Chaneli ya Super Sport na kuwataka wachezaji wa timu hizo kuonyesha uwezo wao kwa sababu ni fursa ya pekee kuonekana katika nyanja ya Kimataifa. Aidha amewataka Watanzania ambao hawajaunganishwa na DStv wafanye hima kununua ving'amuzi ili waweze kushuhudia mechi hizo pamoja na chaneli nyinginezo zinazopatikana katika DStv

Kipindi cha Africa Soccer Show kwa mara ya kwanza kilifanyika LIVE nchini Tanzania. Pichani ni Watangazaji wakifanya mahojiano na Katibu Mkuu wa TFF Bw. Angetile Oseah (katikati).

About Woinde Shizza

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 Comments:

Post a Comment

unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia