Ticker

6/recent/ticker-posts

LIGI YA VODACOM YAINGIA RAUNDI YA PILI: KAGERA SUGAR V JKT OLJORO 0 - 0 HAKUNA MBABE!

Michuano ya Ligi Kuu ya Vodacom kuwania ubingwa wa Tanzania Bara imeingia raundi ya pili iliyoendea Jana (Septemba 19, 2012) kwa timu zote 14 kuumana katika viwanja saba tofauti nchini.

Wakati Simba ilikuwa mgeni wa JKT Ruvu kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, Mtibwa Sugar ilikuwa mwenyeji wa Yanga kwenye Uwanja wa Jamhuri, mjini Morogoro.

Mechi nyingine za ligi hiyo zilizochezwa jana  ni African Lyon vs Polisi Morogoro kwenye Uwanja wa Azam Complex, Dar es Salaam. Nayo Ruvu Shooting ilishuka kwenye Uwanja wake wa Mabatini, Mlandizi kuikabili Mgambo Shooting kutoka Handeni mkoani Tanga.
 
Tanzania Prisons ilicheza kwenye Uwanja wake wa Kumbukumbu ya Sokoine jijini Mbeya kuikabiri Coastal Union ya Tanga wakati Oljoro JKT imeitembelea Kagera Sugar kwenye Uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba. Uwanja wa CCM Kirumba, jijini Mwanza ulishuhudia mechi kati ya wenyeji Toto Africans na Azam.



Baadhi ya waamuzi wa mpira wa leo
 wachezaji wakisalimiana kabla ya mtanange kuanza kuchezwa muda
 waamuzi wa mpira kagera Sugar na Jkt Oljoro

 picha ya Pamoja haikukosa
 Mtanange ukiendelea uwanjani Kaitaba Stadium
 benchi la timu ya Jkt Oljoro
 Wachezaji wa Kagera Sugar na viongozi wao wakitazama mtanange kwa makini
wachezaji wa Akiba wa Kagera Sugar
 
HSANI YA BUKOBASPORTS.COM
Mashabiki.
Ubao ukionesha hakuna mbabe kati yao wawili
Askari nao walikuwepo kwa ulinzi zaidi
Mtanange ukiendelea Kuumia ni jambo lakawaida uwanjani hapa aliumia mchezaji wa kagera Sugar



Kipa wa Kagera Sugar
 Mchezaji wa Kagera sugar aliumia na kutolewa nje


Wakati wa mapumziko.



 
kwa HSANI YA BUKOBASPORTS.COM

Post a Comment

0 Comments