Ticker

6/recent/ticker-posts

BILAL AWAFARIJI MAJERUHI WA MABOMU ARUSHA

 pole mtoto mungu atakusaidia utapona maneno haya makamu wa rais alimwambia mtoto huyu wakati alipotembelea majeruhi katika hospitali ya mounti meru

 mbunge wa jimbo la Arusha mjini katika kati Godbless Lema akiwa na mbunge wa jimbo la Arumeru mashariki Joshua Nassari wakiangalia kanisa ambalo limelipuliwa na bomu hivi leo asubui

 Baadhi ya wananchi wakiwa wanafurahia mara baada ya kuvunja geti la hospitali ya mkoa ambapo awali mlinzi alidai kuwa funguo umepotea huku gari ya majeruhi ikiwa inasubiri kufunguliwa geti ili ipitishe mgonjwa
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr,Mohame Bilal akiwa anawapa pole majeruhi waliolazwa katika hospitali ya mkoa ya Mounti Meru mara baada ya kulipukiwa na bomu wakati wakiwa katika misa ya uzinduzi wakanisa la Mt,Josephy Mfanyakazi katika kata ya Olasiti jijini Arusha
MTU mmoja amekamatwa na anaendelea kuhojiwa na polisi kufuatia mlipuko mkubwa wa bomu lililorushwa kwa waumini wa Kanisa Katoliki jana ambapo watu 66 wamejeruhiwa wakiwamo wanawake 41 na wanaume 25, huku majeruhi wawili hali zao zikiwa mbaya zaidi.

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Magesa Mulongo alimweleza Makamu wa Rais, Dk. Mohamed Gharib Bilal na Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, Said Mwema,naibu waziri wa mambo ya ndani PereiSilima,na naibu waziri wa nishati na madini Stephen Masele wakati walipowatembelea majeruhi waliolazwa katika Hospitali ya Mount Meru jana jioni.
Alisema kati ya majeruhi hao wawili hali zao ni mbaya, huku mmoja akiwa akiwa amepelekwa hospitali ya KCMC kwa matibabu zaidi.

Makamu wa Rais alitarajiwa kuondoka na majeruhi mwingine mtoto ambaye anapelekwa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kwa matibabu zaidi.

Mulongo alithibitisha kwamba aliyefariki katika tukio hilo ni mama mmoja ambaye wa kwanya ya Kimasai ambayo ilikuwa ikiimba kwenye shughuli za uzinduzi wa kanisa hilo.

Akitoa pole kwa wagonjwa waliolazwa pia kwa wale ambao jamaa zao wamepata maradhara kwa tukio hilo, kwa waumini wa Kanisa Katoliki, kwa wakazi wa Arusha na Watanzania kwa ujumla, Dk Bilal alisema tukio hilo ni la aibu na baya sana.

“Tukio hili ni la aibu sana, baya, limeshtusha kutokea hapa nchini, serikali inalaani na itafanya kila linalowezekana kuwatia mbaroni wahusika na tayari imekwishaanza kuhakikisha wahusika wanakamatwa.

“Vyombo vya usalama vimeagizwa kufanya kazi hii usiku na mchana kuhakikisha kwamba wahusika wanakamatwa na wanachukuliwa hatua,” alisema.

Mkuu wa Jeshi la Polisi, Mwema akitokea Dodoma kuhudhuria vikao vya bunge ambako leo Wizara ya Mambo ya Ndani inawasilisha bajeti yake, alielezea tukio hilo kuwa ni la kushutua sana.

“Ni tukio la kushtua, kusikitisha, tumefika eneo la tukio na mpaka sasa mtu mmoja amekamatwa na anaonyesha ushirikiano mzuri wa kutoa taarifa.

“Tukio kama hili sio la mtu mmoja, wapo waliohusika katika kupanga, kuratibu, kushauri, kuchangia gharama na wale waliofanikisha. Hata huyu mmoja aliyekamatwa ni mchango wa ushirikiano wenu, naombeni muendelee kushirikiana na polisi katika kufanikisha uchunguzi huu.

Kwa upande wake, Askofu Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri  Tanzania (KKKT), Dk Alex Malasusa, ambaye aliambatana na Makamu wa Rais kutokea mkoani Shinyanga, alisema amesikitishwa sana na tukio hilo.

Alisema tukio hilo sio la kawaida na limewashtua watu wengi wanaopenda amani lakini amewaomba waendelee kuwa watulivu wakati suala hili linapoendelea kufanyiwa uchunguzi.

“Wakristo tuendelee kuhubiri amani, kuombea amani kwa sababu Mungu wetu ni wa amani,” alisema.

Post a Comment

0 Comments