Ticker

6/recent/ticker-posts

UNESCO yaendesha warsha ya siku moja kujadili Ripoti ya hali ya Elimu na Huduma za Afya ya uzazi, maadili na mahusiano ya kingono kwa Vijana nchini


Mwenyekiti wa TACAIDS Dk. Fatma Mrisho (katikati) akizungumza wakati kufungua warsha siku moja ya mapitio na uhakikisho wa Ripoti ya hali ya Elimu na Huduma za Afya ya uzazi, maadili na mahusiano ya kingono kwa Vijana nchini ambapo warsha hiyo imeshirikisha Taasisi mbalimbali zikiwemo AMREF, UNICEF, Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi kutoka Tanzania Bara na Visiwani, TGNP, Wizara ya Afya na ustawi wa Jamii na nyinginezo. Kushoto ni Abdoul Coulibaly wa UNESCO na kulia ni Mwezeshaji wa Warsha hiyo kutoka Chuo kishirikishi cha Elimu cha Chuo kikuu cha Dar es Salaam (DUCE) Dr. Kitila Mkumbo.
Mwezeshaji wa Warsha hiyo kutoka Chuo kishirikishi cha Elimu cha Chuo kikuu cha Dar es Salaam (DUCE) Dr. Kitila Mkumbo akitoa mwongozo kwa washiriki wa warsha hiyo ambapo katika majumuisho yalioamuliwa kwenye warsha iliyofanyika leo ya kujadili Ripoti ya hali ya Elimu na Huduma za Afya ya uzazi, maadili na mahusiano ya kingono kwa Vijana nchini yatawasilishwa katika mkutano wa Mawaziri utakaohusisha nchi 21 za Afrika Mashariki na Kusini.
Picha juu na chini ni National Program Officer – HIV & Sexuality Education Mathias Herman kutoka UNESCO akichambua mpango wa majukumu ya nchi za Afrika Mashariki na Kusini na kutoa ufafanuzi wa matokeo ya utafiti wa Ripoti ya hali ya Elimu na Huduma za Afya ya uzazi, maadili na mahusiano ya kingono kwa Vijana nchini ambapo ameongeza kuwa nchi inatakiwa kujipanga kwa kusaidiwa na UNESCO pamoja na washirika kuongoza jitihada za kitaifa ambazo zitawawezesha washirika wakubwa ambao ni vijana kushiriki katika mikakati ya kitaifa itakayowasidia vijana nchini kujua mtazamo wao.
Pichani ni Washirki wakifuatilia uchambuzi wa Ripoti uliokuwa ukiwasilishwa na Mathais Herman kutoka UNESCO.
Mwakilishi kutoka Wizara ya Elimu na Ufundi stadi Bw. Raymond Benedict (kushoto) akikata kujua kuhusu mapitio ya Ripoti ya hali ya Elimu na Huduma za Afya ya uzazi, maadili na mahusiano ya kingono kwa Vijana nchini, huduma zinazotolewa na serikali na nini hatma na vijana wameelewa kwa kiwango gani.
Pichani juu na chini washiriki wa warsha ya siku moja iliyoandaliwa na shirika la UNESCO nchini wakichangia maoni yao.Pichani juu Katikati ni Mwenyekiti wa Asasi ya vijana ya Umoja wa Mataifa (YUNA) Lwidiko Edward akiwakilisha vijana na kulia ni Abdoul Coulibaly wa UNESCO
Picha juu na chini ni Washirki wakiendelea kufuatilia yaliyokuwa yakijiri kwenye warsha ya siku moja ya ya mapitio na uhakikisho wa Ripoti ya hali ya Elimu na Huduma za Afya ya uzazi, maadili na mahusiano ya kingono kwa Vijana nchini iliyofanyika leo jijini Dar es Salaam na kufunguliwa na Mwenyekiti wa TACAIDS Dk. Fatma Mrisho.

Post a Comment

0 Comments