Ticker

6/recent/ticker-posts

Umoja wa Mataifa kupitia mpango wa UBRAF waendesha semina kwa watangazaji wa radio za kijamii za Afrika Mashariki


Picha juu na chini ni Mshauri wa Radio Jamii na Mkufunzi wa UNESCO Dar es Salaam Bi. Rose Mwalimu akiendesha majadiliano kuhusu mikakati endelevu itakayowezesha kuihusisha jamii katika program zinazohusu kujikinga na maambukizi ya Virusi vya Ukimwi wakati wa warsha iliyofadhiliwa na mpango wa Unified Budget Result Accountability Frame Work (UBRAF) uliochini ya Umoja wa Mataifa.
Mjumbe wa Kongamano lililofadhiliwa na UBRAF lililohusisha Redio za Kijamii za Afrika Mashariki kutoka Kenya Community Media network (KCOMNET) Njuki Githethwa akiwasilisha ripoti ya maendeleo na ufanisi wa mtandao huo ambao unalenga kujenga fursa ya kitaifa ya kuratibu, kulinda na kusaidia sekta ya vyombo vya habari vya kijamii nchini Kenya wakati wa warsha ya siku mbili iliyoratibiwa na mpango wa UBRAF uliochini ya Umoja wa Mataifa iliyofanyika hivi karibuni Terrat Wilayani Simanjiro Mkoani Manyara.
Picha juu na chini ni Afisa Habari wa Kitengo cha habari cha Umoja wa Mataifa (UNIC) Dar es Salaam Bi. Stella Vuzo akizungumzia umuhimu wa kuwa na mikakati madhubuti ya kushirikishana baina ya Waandishi wa habari na Umoja wa mataifa na pia akafafanua mpango mkakati wa Umoja wa mataifa juu ya usalama wa waandishi wa habari pindi wawapo kazini.
Ambapo amewataka ku-share vipindi na habari mbalimbali na Radio ya Umoja wa Mataifa na kuwafanya wao pia kujulikana kimaifa zaidi.
Bw. Jimmy Okello wa COMNETU akitoa tathmini ya ripoti endelevu za Radio za Kijamii nchini Uganda.
Mwakilishi kutoka Mang’elete Community Radio ya nchini Kenya akizungumzia muelekeo na muafaka wa radio za kijamii na kiwango cha mafanikio kilichofikiwa hadi sasa.
Amos Ochieng wa KCOMNET kutoka Kenya akielezea jinsi watangazaji wa Radio za Kijamii za Jumuiya ya Afrika Mashariki wanavyoweza Ku-share habari kupitia mtandao wa kijamii wa pamoja kwa wakati mmoja.
Baadhi ya wadau mbalimbali kutoka tasnia ya habari waliohudhuria semina iliyohusisha Redio za Kijamii iliyofanyika Terrat wilayani Simanjiro mkoani Manyara hivi karibuni kwa udhamini wa Umoja wa Mataifa kupitia Mpango wa UBRAF.

Pichani juu na chini washiriki wa warsha hiyo iliyowakutanisha Watangazaji wa Radio za Kijamii kutoka Kenya, Uganda, Rwanda na Tanzania wakitoa maoni yao ya namna ya kuboresha uandaaji wa vipindi vyao vya Radio za Kijamii sambamba na vikwazo wanavyokumbana navyo katika kazi zao.

Post a Comment

0 Comments