BREAKING NEWS

Wednesday, April 2, 2014

MENO YA TEMBO 495 YAKAMATWA KATIKA MAENEO MBALIMBALI YA HIFADHI HAPA NCHINI KWA KIPINDI CHA MIENZI MITATU

 Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Wanyamapori kutoka Wizara ya Maliasili na Utalii, Paul Sarakikya,Akiongea na waandishi wa habari jiji Arusha
 waandisi wa habari wakiwa wanamsikiliza kwa makini kaimu mkurugenzi wa idara ya wanyama pori



JUMLA ya meno ya tembo 495 yamekamatwa kwenye maeneo mbalimbali nchini katika kipindi cha miezi mitatu kuanzia Januari hadi Machi mwaka huu.
Aidha watuhumiwa wa ujangili 544 wamefunguliwa mashitaka kwenye mahakama mbalimbali ambapo kesi 62 zimemalizika huku 38 zikiwa bado zinaendelea.
Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Wanyamapori kutoka Wizara ya Maliasili na Utalii, Paul Sarakikya, alibainisha hayo mjini hapa jana alipokuwa akitoa taarifa ya robo mwaka juu ya hali ya ujangili nchini.
Alisema kuwa nyara hizo za serikali zilikamatwa kutokana na doria iliyoendeshwa na watumishi wao waliopo kwenye mapori ya akiba na kikosi cha kuzuia ujangili kwenye maeneo mbalimbali.
Sarakikya alisema kuwa katika kipindi hicho, jumla ya mizoga ya tembo 39 ilionekana ndani na nje ya hifadhi za taifa na mapori ya akiba huku nyama za wanyamapori kilo 1,111 zikikamtwa.
“Aidha meno ya tembo yaliyokamatwa yalikuwa katika hali mbalimbali ambapo mazima yalikuwa 171, vipande 22 vya meno ya tembo ghafi, vipande 302 vya meno ya tembo yaliyochakatwa yenye jumla ya kilo 662.62 yalikamatwa,” alisema.
Alisema kuwa pia walifanikiwa kukamata silaha 11 ikiwemo bunduki ya rasharasha 1, rifle 3, shotgun 2, gobore 5 pamoja na risasi saba za aina mbalimbali.
“Mali na vifaa vingine vilivyokamatwa ni pamoja na magari matano ambavyo vilikamatwa kwa kuhusika kwenye vitendo vya ujangili hasa wa meno ya tembo, ng’ombe 2,663 walioingia kwenye hifadhi pamoja na msumeno mmoja wa kukata mbao na mbao 745,” alisema Sarakikya.
Alisema kati ya kesi 124 zilizofunguliwa kwenye mahakama tofauti nchini, 62 zilizokuwa na washitakiwa 85 zilimalizika kwa watuhumiwa kulipa faini ya zaidi ya sh milioni 25.5.
Sarakikya alisema meno ya tembo waliyokamata yalitokana na matukio ya siku za nyuma, jambo alilodai walilibaini kutokana na meno hayo kuwa yamebadilika rangi kwa kuchimbiwa ardhini muda mrefu huku mengine yakimeguka.
Taarifa hii imekuja siku moja baada ya watu sita wanaodhaniwa kuwa ni majangili kukamatwa na meno ya tembo 53 yenye jumla ya kilo 169.7 wakiwa na silaha aina ya SMG yenye magazine tatu kwenye Kijiji cha Kiomboi wilayani Manyoni mkoani Singida.

Share this:

Post a Comment

unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia

 
Back To Top
Copyright © 2014 MOUNT KILI NEWS. Designed by OddThemes | Distributed By Gooyaabi Templates