JUMLA ya shilingi Milioni 160 zimechangwa
katika harambee ya kuchangia ujenzi wa hosptali maalumu kwa ajili ya kina mama na watoto
katika kata ya Sombetini jijini arusha .
Harambee hiyo iliongozwa na Diwani wa kata ya Mlangariini
Mathias Manga ambaye pia ni mfanyabiashara maarufu wa madini jijini Arusha ,ambapo alitoa kiasi cha shilingi milioni 20 na kufuatiwa na watu mbalimbali walioalikwa.
Harambee hiyo iliongozwa na Diwani wa kata ya Mlangariini
Mathias Manga ambaye pia ni mfanyabiashara maarufu wa madini jijini Arusha ,ambapo alitoa kiasi cha shilingi milioni 20 na kufuatiwa na watu mbalimbali walioalikwa.
Manga alisema kuwa
ujenzi wa hospitali hiyo utasaidia kupunguza kero kwa akina mama ya kufuata
huduma ya matibabu umbali mrefu iliyokuwa ikisababisha wengi wao kujifungulia njiani .
Alisema
lengo la harambee hiyo ni kupatikana kwa kiasi cha shilingi milioni 200 ambazo
zingewezesha kukamilisha ujenzi wa hospitali hiyo inayomikiliwa na kanisa katoliki Parokia ya moyo mtakatifu wa Yesu kata
ya Sombetini .
Aidha
diwani Manga alisema kuwa ameamua kushiriki katika harambee hiyo kwa kuwa
anajua kuwa wajibu wa kiongozi yoyote yule ni kushiriki huduma za kijamii
pasipo kuzikwepa au hata kutoa ahadi ambazo hazitekekelezeki katika jamii.
“ndugu
zangu sisi wanasiasa tumekuwa tukisifika sana kutoa ahadi ambazo hazitekelezeki
ila kwa upande wangu napenda niwahakikishie yakuwa kiongozi si kuahidi tu bali
ni kutekeleza na jamii inafarijika kuona kiongozi anakuwa mstari wa mbele
kuhudumia jamii’’alisema Manga
Diwani huyo ambaye alikuwa mgeni rasmi kwenye hafla hiyo alisema kuwa kiongozi anatakiwa kuhakisha harakati zote za kuiletea jamii maendeleo zinapiga hatua hususani kwa mambo muhimu kama ujenzi wa shule , Hosptali ,barabara pamoja na Uboreshaji wa Miundo mbinu.
Kwa upande wake Padri wa parokia hiyo Padri Moses Mwaniki Gitau amewaondoa shaka wakazi waishio katika kata ya Sombetini jjini Arusha kwa ujumla kuwa hospitali hiyo ikikamilika itakuwa mkombozi kwo kwa kuhudumia wakazi wote bila ya kujali itakadi za kidini ama kisiasa na wale wasiojiweza watapewa kipaumbe cha kupata matibabu.
Wakati huo huo mwenyekiti wa harambee hiyo Joseph Masawe alisema imefika muda muafaka kwa watanzania kujitolea kwa hali na mali katika kujenga mahitaji muhimu yaliyopo ndani ya jamii ikiwemo shule, Vituo vya
afya na sio kutegemea wafadhili kutoka nje.
Hata hivyo ametoa wito kwa jamii nchini kubadika kimtazamo kuchangia miradi yenye tija ya maendeleo kwa jamii sio kuchangia vitu vye manufaa kwa watu wachache kama sherehe sambamba na mambo ya anasa ambayo hayana faida kwa jamii.
Diwani huyo ambaye alikuwa mgeni rasmi kwenye hafla hiyo alisema kuwa kiongozi anatakiwa kuhakisha harakati zote za kuiletea jamii maendeleo zinapiga hatua hususani kwa mambo muhimu kama ujenzi wa shule , Hosptali ,barabara pamoja na Uboreshaji wa Miundo mbinu.
Kwa upande wake Padri wa parokia hiyo Padri Moses Mwaniki Gitau amewaondoa shaka wakazi waishio katika kata ya Sombetini jjini Arusha kwa ujumla kuwa hospitali hiyo ikikamilika itakuwa mkombozi kwo kwa kuhudumia wakazi wote bila ya kujali itakadi za kidini ama kisiasa na wale wasiojiweza watapewa kipaumbe cha kupata matibabu.
Wakati huo huo mwenyekiti wa harambee hiyo Joseph Masawe alisema imefika muda muafaka kwa watanzania kujitolea kwa hali na mali katika kujenga mahitaji muhimu yaliyopo ndani ya jamii ikiwemo shule, Vituo vya
afya na sio kutegemea wafadhili kutoka nje.
Hata hivyo ametoa wito kwa jamii nchini kubadika kimtazamo kuchangia miradi yenye tija ya maendeleo kwa jamii sio kuchangia vitu vye manufaa kwa watu wachache kama sherehe sambamba na mambo ya anasa ambayo hayana faida kwa jamii.
0 Comments
unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia