ICTR YAHITIMISHA KUPOKEA USHAHIDI MAALUM KATIKA KESI YA BIZIMANA


Mahakama ya Kimataifa ya Mauaji ya Kimbari ya Rwanda (ICTR) Jumatatu ilihitimisha upokeaji wa ushahidi maalum katika kesi inayomkabili mtuhumiwa wa mauaji ya kimbari ambaye bado anasakwa na mahakama hiyo, Augustin Bizimana, Waziri wa zamani wa Ulinzi wa Rwanda.
 
‘’Naomba niwajulishe kwamba upokeaji wa ushahidi maalum katika kesi ya Bizimana uliendelea leo (Jumatatu) asubuhi kwa kupata ushahidi kutoka kwa shahidi wa mwisho ambaye pia amehitimisha ushahidi wake leo.Hivyo basi kufuatia hatua hiyo, upokeaji ushahidi huo umehitimishwa,’’ alieleza Msemaji wa ICTR, Roland Amossouga.
 
Bizimana anashitakiwa kwa makosa ya mauaji ya kimbari, kula njama kutenda makosa hayo, uhalifu dhidi ya binadamu na uhalifu wa kivita.
 
Kesi nyingine mbili za aina hiyo ambazo ushahidi wake umeshapokelewa ni pamoja na ile ya mtuhumiwa anayesakwa vikali na anayesadikiwa kuwa ndiyo mfadhili wa mauaji ya kimbari, Felicien Kabuga na Protais Mpiranya, aliyekuwa Kamanda wa Kikosi cha Walinzi wa   Rais.
 
Utaratibu wa kupokea ushahidi katika kesi ya mshitakiwa ambaye bado hajakamatwa umewekwa ili kuhifadhi ushahidi husika uweze kutumika pindi mshitakiwa akitiwa mbaroni hapo baadaye.
 
Wakili wa Zamu wa Bizimana, Yitiha Simbeye aliita jumla ya mashahidi watatu kwa ajili ya utetezi wa mteja wake. Utetezi katika kesi ya Biziamana ulianza Mei 14, 2012.

About Woinde Shizza

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 Comments:

Post a Comment

unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia