Rais na Msajili wa Mahakama ya
Kimataifa ya Mauaji ya Kimbari ya Rwanda (ICTR) wanaendelea kuhaha
kutafuta nchi za kuwapokea washitakiwa walioachiwa huru na mahakama
hiyo.
Rais wa ICTR, Jaji Vagn Joensen aliliambia Shirika la Habari la
Hirondelle kwamba ‘’ Msajili na mimi tutazidisha juhudi zetu za
kidiplomasia kutafuta nchi zitakazofaa kuwapokea waliochiwa huru.’’
‘’Katika hutuba yangu niliyoitoa mbele ya Baraza la Usalama la Umoja
wa Mataifa Juni 8, mwaka huu, nililiomba Baraza la Usalama kutoa wito
kwa nchi zote kushirikiana nasi katika kulipatia ufumbuzi tatizo
hili.’’alisema.
ICTR inatarajiwa Jumatatu ijayo kukabidhi baadhi ya majukumu yake kwa
taasisi mpya itakayorithi kazi zinazobakia za mahakama hiyo
ijulikanayokamaInternational Residual Mechanism (IRM).
Tatizo la kupata nchi za kuwapokea washitakiwa wanaoachiwa huru na
ICTR bado linaumiza vichwa vya wakuu wa ICTR licha ya wito mbalimbali
uliokuwa unatolewa na mahakama hiyo siku za nyuma.
‘’Ugumu utabaki kuwa uleule, yaani kukosa utayari wa nchi kuwapokea
wanaoachiwa huru katika ardhiyao, kwa sababu wanazozifahamu wenyewe,’’
Msemaji wa ICTR, Roland Amoussouga aliiambia Hirondelle, Novemba mwaka
jana.
Mahakama ya Rufaa ya ICTR imeshathibitisha kuachiwa huru kwa watu
watano lakini bado hawajapata nchi za kuwapokea.Watu hao ni pamoja na
jenerali mmoja wa jeshi, mawaziri watatu na shemeji wa Rais wa zamani
waRwanda, marehemu Juvenal Habyarimana.
Wote hao wanataka kuungana na familia zao zinazoishi Ulaya, wengi wao wakiwa wameshapata urai wa nchi hizo.
0 Comments
unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia