KESI YA SABA TOKA ICTR YAKUBALIWA KUHAMISHIWA RWANDA

Mahakama ya Kimataifa ya Mauaji ya Kimbari ya Rwanda (ICTR) Jumatatu ilikubali maombi ya mwendesha mashitaka wa mahakama hiyo kuhamishia nchini Rwanda kesi ya mshitakiwa, Aloys Ndimbati.
 
Hii ni kesi ya saba toka ICTR kupelekwa kusikilizwa katika mahakama za Rwanda.
 
Katika uamuzi wake, Mahakama iliyokuwa inaongozwa an Jaji Vagn Joensen imemwamuru mwendesha mashitaka wa ICTR kumkabidhi Mwendesha Mashitaka Mkuu wa Rwanda, nyaraka zote zinazounga mkono mashitaka dhidi ya mtuhumiwa ambaye bado anasakwa na mahakama hiyo, mapema iwazekanavyo.
 
Amri hiyo inatakiwa kutekelezwa katika kipindi cha siku 30 tangu kutolewa kwa amri ya mwisho ya kuhamishwa kwa kesi hiyo. 
 
Mahakama ilielezea matumaini yake kwamba ‘’Jamhuri ya Rwanda, kwa kubali kesi toka ICTR, itatekeleza kwa vitendo ahadi iliyotoa juu ya kuzishughulikia kesi hizo kwa nia njema, uwezo ulio nao na utayari wa kuzingatia viwango vya juu vya kimataiafa vya utendaji haki.’’
 
Ndimbati, Meya wa zamani wa wilaya ya Gisovu, mkoa wa Kibuye, Magharibi ya Rwanda, anashitakiwa kwa mauaji ya kimbari, kula njama za kufanaya mauaji hayo, uchochezi na uhalifu dhidi ya binadamu kwa kuua, kuteketeza kizazi, ubakaji na utesaji.   
 

About Woinde Shizza

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 Comments:

Post a Comment

unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia