MKUU WA WILAYA YA HAI ATEMBELEA MAKAO MAKUU YA POLISI WILAYANI HUMO AKUMBANA NA MATATIZO LUKUKI YANAYOKIKABILI KITUO HICHO
mkuu huyo wa wilaya Novatus Makunga akiwasili akisindikizwa na mkuu wa polisi wilayani hao OCD Isaya Mbughi na maofisa wengine
Mkuu wa wilaya ya Hai mkoani Kilimanjaro Mhe.Novatus Makunga leo amefanya ziara katika makao makuu ya jeshi la polisi wilayani Hai mkoani Kilimanjaro na kuongea na askari polisi wa wilaya hiyo
askari wakiwa wanamsikiliza kwa makini mh.Novatus Makunga Dc wa Hai
maafande mbalimbali wakitoa maoni yao katika mkutano wao na mkuu huyo wa wilaya
Jeshi la Polisi wilayani Hai linakabiliw ana matatizo makubwa ya
ukosefu wa mafuta pamoja na uboifu
wa magari hali inayochangia jeshi
hilo kushindwa kukabiliana na uhalifu uliokithiri wilayani humo
Hayo ameelezwa
jana na askari polisi wa wilaya
hiyo wakati wa mkutano wao wa kwanza na mkuu wa wilaya hiyo Novatus Mhando Makunga alipotembelea makao
makuu ya polisi wilayani humo
Miongoni
mwa chanagmoto hizo ni ukosefu wa nyumba
za makazi ya askari, askari kutopandishwa vyeo kwa miaka mingi pamoja na askari kukosa vitendea kazi yakiwemo makaratasi
Kutokana
na hali hii Mkunga ameahidi kuzibeba na kuzifikisha ngazi
ya juu ya jeshi hilo pamoja na serikali
ya mkoa
Askari
hao wamemweleza Mkuu huyo wa wilaya kuwa wamekuwa
wakitupiw alawama kutokana na kushindwa kufika maeneo ya matukio ya
uhalifu kutokana na ubovu wa magari mawili yaliopo katika kituo hicho pamoja na kukosa mafuta
Wametoa mfano
kwamba pindi kunapoitokea taarifa za uhalifu mkuu wa polisi wilayani
humo ama ofisa upelelezi wanalazimika
kutoa fedha zao mfukoni ili kununua mafuta ndipo askari waweze kufika eneo la tukio
Hali hii
haitendi haki kwa askari hao kununua mafuta wakati wakitumikia taifa
huku seriali ikiwa kimya katika kutatua matatizo hayo ya kushindw akutoa fedha za
uendeshaji pamoja na magari ya uhakika
ili kukabiliana na uhalifu
Wamesema wilaya ya hai inakabiliwa na uhalifu
mwingi ukiwemo wa biashara ya gongo,
ujambazi pamoja na migogoro kati ya wafugaji na wakulima
Aidha askari
hao pia wamemweleza mkuu wa wilaya
makunga kwamba kuekuwepo na ufinyu wa ofisi ambapo mfano
askari wa kikosi cha usalama
barabarani wapatao 30 hutumia ofisi mmoja yenye ukubwa wa mita za mraba saba kwa kumi
Pia kituo
hicho cha polisi hakina samani mfano askari polisi hukaa kwenya mawe wakati wakishughulikia
masuala mbalimbali ya kesi
Baadhi ya
askari wamemweleza mkuu huyo wa wilaya kuwa jeshi la polisi wilayani humo linaweza
kuingia katika madhara na vishawishi vingi vibaya kutokana na kutegemea misaada
ya mafuta kutoka kwa wafanyabiashara wakubwa wilayani humo vishawishi ambavyo ni
hatari kwa utendaji wao wa kazi za
kiaskari
Baadhi yao
wamesema wamekuwa katika jeshi hlo kwa zaidi yamiaka 20 bila kuajiriwa na badala yake wamekuwa vibarua miaka yao yote hasa askari
wa ngazi ya chini
Kuhusu suala
la likizo mkuu wa polisi wilayani humo SP Isaya Mbughi amemweleza mkuu wa
wilaya makunga kwmaba askari wengi wilayani huo wanashindwa kwenda likizo
kutokana na baadhi yao kuuza likizo zao na kushindwa kwenda maeneo walikozaliwa badala yake wamekuwa wakililaumu
jeshi la polisi
OCD Mbughi
alisema lipo tatizo kubwa la biashara ya
gongo linalochangiwa na baadhi ya viongozi wa vijiji wanaoshiriki katika
biashara hiyo wilayani humo
Akizungumza
na askari polisi hao Mkuu wa wilaya Makunga
aliwataka waimarishe mshikamano katika kukabiliana na uhalifu liiwemo tatizo la gongo
Mkunga
alisisitiza kuwa askari polisi ni lazima
wawe kitu kimoja ili kuweza kudhibiti
uhaliufu wilaya ni humo
Kuhusu
mjadala wa mabadiliko ya katiba, Makunga aliwataka askari polisi hao kushiriki
kikamilifu kutoa changamoto
zitakazosaidia kasoro zilizopo katika
uendeshaji wa jeshi hilo zinazopaswa kuingizwa Katika katiba hiyo
Amesema
katiba ndiyo nguzo kuu ya kuongoza
masuala mbalimbali ya nchi hivyo ni wajibu wa askari polisi kuhakikisha masuala
yao yote muhimu yanaingizwa katika katiba hiyo







0 Comments:
Post a Comment
unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia