MDAHALO

Wafanyakazi wa radio sunrise wakiongozwa na severinus mwijage wakifatilia kwa makini mdahalo ulikuwa umeandaliwa na ANGONET uliokuwa unafanyika katika hotel ya Golden rose jijini hapa
mtoa mada ambaye ni mkuu wa wilaya ya mbeya Noman Sigalla

HALMASHAURI mbalimbali ndani ya Nchi ya Tanzania zimetakiwa kyuhakikisha kuwa zinakuwa wazi hasa wakati watakapokuwa wanapanga bajeti ili kuziepusha na matatizo mbalimbali

Hayo yameelezwa na  mwanaharakati wa mambo mbalimbali hapa nchi BwMarcos Albwane wakati akizungumza katika mdahalo kuhusu uwazi na uwajibikaji  katika kusimamia rasilimali za nchi

Alisema kuwa uwazi ni kipengele muhimu sana na kwa hali hiyo ni vema hata halmshauri nazo zikatekeleza mpango huo tofauti na sasa ambapo kuna changamoto lukuki sana

Aliongeza kuwa endapo kama hali hiyo itafanikishwa ndani ya halmashauri hasa wakati wa upangaji wa bajeti basi hali hiyo itachangia kwa kiwango kikubwa sana hata kwa watendaji wa halmashauri kuwa na dhana ya uwajibikaji wa hali ya juu sana

Alisema kuwa dhana hiyo pia inaenda sanjari na dhana ya uwajibikaji kwa viongozi wa  halmashauri  kwa kuwa utaweza hata kuboresha utendaji wa Serikali kuu na serikali za mitaa hivyo kuendeleza kukua na kuimarisha utawala bora

Alifafanua kuwa katika Serikali za mitaa ni muhimu sana kuwezesha ushiriki wa wananchi katika mchakato mzima wa kuweza kufanya maamuzi ambapo kwa sasa tayari Serikali imeshaweza kuongeza idadi ya uwajibikaji

Hataivyo mdahalo huo uliwashirikisha wadau zaidi ya 500 kutoka katika maeneo mbalimbali ya Arusha huku lengo likiwa ni kujadili juu ya rasilimali za taifa ambazo wananchi wanatakiwa kuzitambua


About Woinde Shizza

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 Comments:

Post a Comment

unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia