KAMPENI YA ULINZI WA MTOTO HAI WAPUNGUZA ONGEZEKO LA WATOTO WA MITAANI


Kampeni  kubwa kwa jamii dhidi ya ulinzi wa mtoto katika wilaya ya Hai mkoani Kilimanjaro imewezesha kupungua kwa vituo vya kulelea yatima na wanaoishi katika mazingira magumu kutoka 22 hadi 7 na pia kuwarudisha watoto 150 katika familia zao katia ya mwaka 2010 na 2012 wilayani humo.

Hayo yameelezwa na Afisa wa maendeleo ya jamii katika halmashauri ya wilaya ya Hai Bi Restina Mwasha wakati ujumbe wa maofisa wa Mfuko wa Umoja wa mataifa wa watoto,UNICEF ulipokutana na mkuu wa wilaya hiyo Bw Novatus Makunga ofisini kwake wilayani humo.

Bi Mwasha ameeleza kuwa hivi sasa kiasi cha uelewa wa masuala yanayohusu ulinzi wa mtoto katika wilaya ya Hai imefikia asiliamia 85 ingawa bado jamii pamoja na mfumo uliopo hajaweza kuchululia kwa uzito unaotakiwa masuala ya mtoto.

Amefafanua kuwa baadhi ya vituo vya kulelea watoto yatima na wanaoishi katika mazingira magumu vimekuwa vikianzishwa zaidi kwa lengo la kuwanufaisha wamiliki wa vituo hivyo kuliko kutatua matatizo ya watoto.

Ameeleza kuwa mkakati huo ulichukuliwa kutokana na kushamiri kwa uanzishwaji wa vituo vya watoto yatima kuanzia mwaka 2010 na hivyo nguvu zilielekezwa katika uelimishaji wa jamii kuhusu suala zima la ulinzi wa mtoto.

Ameeleza kuwa kampeni hiyo ililenga katika kupunguza idadi ya watoto wanaolelewa katika vituo vya watoto yatima,kudhibiti vituo vinavyoendeshwa kwa kiwango cha chini na kupunguza vitendo ukatili wa watoto.

Bi Mwasha ameeleza kuwa zaidi ya masuala 587 yanayohusu ukatili wa watoto yalishughulikiwa na baadhi kutatulia na mengine kupelekwa katika ngazi ya kisheria kati ya mwezi Mei  2010 mpaka machi 2012.

Ametaja baadhi ya matukio kuwa ni pamoja na vipigo,ubakaji,usafirishaji kwa ajili ya kufanyishwa kazi,wizi wa watoto,ujauzito,kuozwa,Lugha chafu na ajira mbaya.

Bi Mwasha ameeleza kuwa wameweza kuendesha mafunzo kwa wadau mbalimbali  ya ulinzi wa mtoto wakiwemo waalimu 342,wauguzi 40,polisi 76,maofisa magereza 2,wasikilizaji masahauri wa kata 14

katika kuimarisha zaidi mkakati wa ulinzi kwa mtoto ameeleza kuwa mbali na timu ya wilaya lakini pia tayari  wameanzisha timu za  ulinzi katika ngazi ya kata kumi  na vijiji 55 huku kukibakiwa na uundwaji wa timu nyingine katika kata mpya 4 na vijiji vipya 5

Hata hivyo Bi Mwasha ameeleza kuwa bado wanakabiliwa na changamoto kubwa ya ukosefu wa  ofisi ya kutosha kuweza kusikiliza kwa faragha masuala ya watoto pamoja na ukosefu wa fedha za kutosha katika katika bajeti

Aidha Bi Mwasha amebainisha changamoto nyingine wanayokutana nayo ni dosari katika fomu namba ya polisi inayotolewa kwa ajili ya matibabu kutokuwa na sehemu ya jina kamili,cheo na taasisi ya daktari anayemuhudumia mtoto aliyeumizwa.

Hata hivyo ameeleza kuwa baadhi ya watoto wamekuwa wakikumbana na mateso pamoja na kwamba wanatoka katika familia zenye uwezo,masuala ya wataoto kudhulumiwa mali na ndugu na baada ya kufariki kwa wazazi wao lazima iwe ajenda katika ulinzi wa mtoto

Kwa upande wake kiongozi wa ujumbe huo wa Unicef  bi Mona Aika ameeleza kuwa wilaya ya Hai imekuwa na mafanikio makubwa zaidi kutokana na utafiti uliendeshwa na mfuko huo katika wilaya za Magu,Temeke na Hai kwa lengo la  kuongezea nguvu mfumo wa mpangilio kwa ulinzi wa mtoto nchini.

About Woinde Shizza

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 Comments:

Post a Comment

unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia