WAFANYAKAZI WA TANZANITE ONE KUBORESHEWA MASLAYI

UONGOZI wa Kampuni ya TanzaniteOne ya madini ya Tanzanite iliyopo Wilayani Simanjiro Mkoani Manyara imesaini mkataba wa kuboresha hali na maslahi ya wafanyakazi wa kampuni hiyo.

Mkataba huo umefanyika baada ya Majadiliano ya muda mrefu hatimaye menejimenti ya kampuni hiyo ikasaini mkataba wa Kuboresha maslahi ya wafanyakazi kupitia Chama Cha Wafanyakazi wa Migodi (Tamico).

Katika kutia saini mkaataba huo juzi,kampuni ya TanzaniteOne iliwakilishwa na Mkurugenzi wake Ndugu Wessel  Morais na Ofisa rasilimali watu Johnson Mwani na Tamico iliwakilishwa na Katibu mkuu Hassan Ameir,Katibu Tamico Kanda,Juma Bwikitia.

Kwa upande wa wafanyakazi wa TanzaniteOne waliwakilishwa na Mwenyekiti wa Tamico wa Tawi hilo Raphael Alex Ombade,Katibu wa Tawi,Richard Nyanginywa na wajumbe wote wa tawi la Tamico Tanzanite One.

Akizungumza baada ya kutia saini kwenye mkataba huo,Morais alisema kuwa ana heshimu  na kuthamini uwepo wa Chama Cha wafanyakazi migodini Tamico ambacho kinatetea maslahi ya wafanyakazi wa kampuni hiyo.

“Migongano na mitazamo tofauri ni sehemu ya kazi na tatizo lolote litakalojitokeza liwasilishwe mezani na Tamico kwa ajili ya majadiliano ya pamoja na kuweza kufikiwa muafaka wa pamoja,” alisema Morais.

Katibu Mkuu wa Tamico Hassan Ameir alisifu na kupongeza hatua iliyofikiwa na tawi kwa ushirikiano mkubwa wa TanzaniteOne nakuthamini umuhimu wa kukaa meza moja kwa majadiliano kwani njia hiyo hupunguza migogoro mingi.

“Viongozi wa wafanyakazi mzidishe bidii,juhudi na maarifa katika uzalishaji ili kuongeza tija na ufanisi shemu ya kazi na kupata nguvu ya kudai maslahi bora zaidi kwani huwezi kumkamua ng’ombe maziwa bila kumlisha vizuri,” alisema Ameir.

Naye,Katibu wa Tamico Kanda ya Kaskazini Juma Saidi Bwikitia alitoa shukrani zake za dhati kwa wote waliohusika kwa namna moja au nyingine kuhakikisha kuwa mkataba huo unafanikiwa kutiwa saini.

“Naziomba pande zote zilizosaini mkataba kuuheshimu na kuutekeleza kwa vitendo kama taratibu za Kisheria zinavyosema na pande wowote kutokwenda kinyume na yale waliyokubaliana ili kudumisha mahuisiano ya ajira kwa mujibu wa Sheria,” alisema Bwitia.
 

About Woinde Shizza

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 Comments:

Post a Comment

unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia