OCAMPO ASHINIKIZA AL-BASHIR KUKAMATWA, KESI YA MUNYAGISHARI YAPELEKWA RWANDA

Mwendesha mashitaka wa Mahakama ya Kimataifa ya Makosa ya Jinai, wiki hii alilihutubia Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa juu ya hali ilivyo nchini Sudan na kulitaka kutafuta mbinu za kumkamata Rais Omar Al-Bashir na viongozi wengine nchini humo, ilihali Mahakama ya Kimataifa ya Mauaji ya Kimbari ya Rwanda iliamuru kuhamishiwa nchini Rwanda kesi inayomkabili Bernard Munyagishari. 
ICC
Ocampo ashinikiza kukamatwa kwa Al-Bashir: Mwendesha mashitaka wa Mahakama ya Kimataifa ya Makosa ya Jinai, Jumanne wiki hii alilitaka Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kutafuta mbinu za kuwakamata viongozi nchiniSudan, akiwemo Rais Omar Al-Bashir. Akilihutubia Barazahilo, Ocampo alisisitiza kuwa kitendo cha serikali yaSudankukataa kumkamata Al-Bashir kunatoa changamoto ya moja kwa moja juu ya mamlaka lililonalo Barazahilo. Siku moja kabla ya kulihutubia Barazahilo, mwendesha mashitaka huyo aliongea na mkosanyiko hukoNew York, ambapo alipendekeza nchi zinazompokea Al-Bashir zinyimwe misaada,kamanjia mojawapo ya kushinikiza kukamatwa kwake. Malawi Jumatatu ilitangaza kumkamata Rais huyo waSudankamaatahudhuria kikao cha wakuu wa nchi barani Afrika kitakachofanyika nchini humo mwezi ujao.
Mawakili wa Gbagbo waomba kusogezwa mbele kesi ya mteja wao: Mawakili wa aliyekuwa Rais wa Ivory Coast Laurent Gbagbo Alhamisi wiki hii waliiomba Mahakama ya Kimataifa ya Makosa ya Jinai kuahirisha hadi siku nyingine kikao cha kuchambuakamamakosa yanayomkabili mteja wao yanastahili kuthibitishwa. Awali, kikao hicho kilikuwa kimepangwa kufanyika Juni 18. Mawakili hao walidai kuwa hali ya kiafya ya mteja wao imemfanya ashindwe kutoa mchango mahususi katika maadalizi ya kikao hicho. Mkuu huyo wa zamani wa nchi ambaye ni wa kwanza kushitakiwa katika mahakama hiyo alifikishwa kizimbani kwa mara ya kwanza Disemba 5, mwaka jana ambapo alifahamishwa makosa yatakayomkabili ya uhalifu dhidi ya binadamu yanayodaiwa kutendeka chini mwake kati ya Disemba 16, 2010 na Aprili 12, mwaka jana. 
ICTR
Kesi ya Munyagishari yahamishiwaRwanda: Mahakama ya Kimataifa ya Mauaji ya Kimbari ya Rwanda Jumatano ilikubaliana na maombi ya upande wa mashitaka na kuamuru kesi ya mshitakiwa wa mauaji ya kimbari Bernard Munyagishari ihamishiwe nchiniRwandakwa ajili ya kusikilizwa. Jopo la majaji watatu walibainisha kuwa katika miaka ya hivi karibuni,Rwandaimefanya mabadiliko makubwa katika sheria zake na imeonyesha uwezo na utayari wa kusikiliza kesi zote zinazohamishiwa nchini humo kutoka katika mahamakama hiyo. Munyagishari anashitakiwa kwa makosa ya mauaji ya kimbari, kula njama kutenda mauaji hayo, kama kosa mbadala, mauaji na ubakaji,kamamakosa ya uhalifu dhidi ya binadamu.
Kesi ya Ngirabatware yaanza tena:  Kesi inayomkabili aliyekuwa Waziri wa Mipango nchiniRwanda, Augustin Ngirabatware ilianza tena kusilizwa Jumanne wiki hii. Upande wa mashitaka uliita shahidi wake wa mwisho ambaye ni mwanadiplomasia kutokaNigeria. Shadidi huyo ameletwa kupinga utetezi wa mshitakiwa kuwa hakuwepo nchiniRwandakati ya Aprili 23 na Mei 23, 2012.  Mahakama baadaye iliahirisha mahojiano ya utetezi kwa shahidi huyo hadi Julai 2.
RWANDA
Mugesera atinga mahakamani bila wakili wake: Jumatatu wiki hii, Msomi waKinyarwanda,LeonMugesera, alifika katika Mahakama Kuu mjiniKigalibila kuongozana na wakili wake. Anapinga uamuzi wa kumkatalia kucheleweshwa kesi yake. Kufuatia Mugesera kukosa uwakilishi wa kisheria, mahakama iliahirisha shaurihilohadi Juni 11.
WIKI IJAYO
 ICC
Jumatatu na Jumanne kutakuwepo na vikao vya kujadili tarehe itakayofaa kuanza kusikilizwa kwa kesi zinazowakabili Wakenya wanne wanaotuhumiwa kuhusika katika makosa yaliyotokana na vurugu baada ya uchaguzi mkuu wa rais nchini Kenya Disemba 2007.
Siku moja baadaye (Jumatano) majaji wa mahakama hiyo watasikiliza hoja za upande wa mashitaka na utetezi juu ya adhabu anayostahili kupewa kiongozi wa waasi, Thomas Lubanga, ambaye ametiwa hatiani kwa makosa ya uhalifu dhidi ya binadamu.
RWANDA
Mshitakiwa wa mauaji ya kimbari, Leon Mugesera, anatarajiwa kufika tena mahakamani Jumatatu kujua mustakabali wa kesi yake.

About Woinde Shizza

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 Comments:

Post a Comment

unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia