MJI MDOGO WA NGARAMOTONI WAONGOZA KWA UCHAFU ARUSHA

MJI mdogo wa  Ngaramtoni Wilayani Arusha Vijijini upo hatarini kukumbwa na Magonjwa ya Mlipuko (Kipindupindu)hasa katika nyakati hizi za Mvua kali kutokana na baadhi ya maeneo ndani ya mji huo kukumbwa na uchafu

Akiongea na Libeneke la kaskazini mkazi wa eneo hilo  kwa niaba ya wananchi wa eneo hilo  James Mrutu alisema kuwa mji huo kwa sasa una uchafu mwingi sana hali ambayo inahatarisha afya za wakazi wa eneo hilo

Alisema kuwa hapo awali kulikuwa na utaratibu mzuri sana wa kuzoa taka katika maeneo mbalimbali lakini kwa sasa utaratibu huo haufuatwi na badala yake taka zimekuwa zikisagaa ovyo huku zikitoa harufu mbaya sana

Aliongeza kuwa  endapo kama hali hiyo ya uzoaji wa taka kwa haraka haitaweza kufuatwa basi taka hizo zinaweza kusababisha matatizo makubwa ya magonjwa ya mlipuko kama vile homa ya matumbo(TYPHOID)na Kipindupindu jambo ambalo nalo litakuwa ni chanzo kikubwa sana cha umaskini

Aliziomba mamlaka husika kuhakikisha kuwa zinazingatia zoezi zima la uzoaji wa Taka ambapo hapo awali kulikuwa na utaratibu wa kutupa taka kwa kutumia magari maalumu tofauti na sasa ambapo wananchi walio wengi wanakusanya taka hizo kila siku huku gari nalo likiwa halina utaratibu wa kupita mara kwa mara .

Awali diwani wa eneo hilo bw David Kinisi alithibitisha kuwepo kwa changamoto hiyo ya kukithiri kwa ongezeko kubwa sana la uchafu katika mji mdogo wa Ngaramtoni na kusema kuwa wahusika wanaweka mji huo pabaya

  kinisi alifafanua kuwa endapo kama hali hiyo itaendelea ni wazi kuwa Madhari ya mji huo itakuwa na mtizamo wa tofauti sana hali ambayo nayo itachangia kukithiri kwa magonjwa,pamoja na umaskini mkubwa ambao unaletwa na uchafu

Alizitaka mamlaka husika kuhakikisha kuwa zinafanya mara moja zoezi hilo na kuweza kuokoa madhari ya Mji huo wa Ngaramtoni kwa kuwa hapo awali Mji huo ulikuwa ni miongoni mwa Miji yenye sifa za usafi sana katika halmashauri hiyo  ya Arusha Vijijini.

About Woinde Shizza

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 Comments:

Post a Comment

unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia