MSANII DIAMOND KUPAMBA REDS MISS ARUSHA
Msanii Diamond katika pozi
Wakati wanyange wa kinyanganyiro cha Reds miss Arusha wakiingia
kambini Jana msanii wa muziki wa kizazi kipya(bongo Flava)Naseeb Abdull
alimaarufu Diamond anatarajiwa kupamba shindano hilo linalotarajiwa
kufanyika June 23 jijini hapa.
Akiongea na waandishi wa habari muandaaji wa shidano hilo ambaye pia ni mkurugenzi wa mwandago investment ltd Faustoin Mwandago alisema kuwa shindano hilo linatarajiwa kufanyika katika ukumbi wa mount meru hotel na litakuwa ni onyesho la kukata na shoka.
Alisema kuwa jumla ya warembo 20 kutoka vitongoji vinne vya mkoa wa Arusha wameingiaa kambini kujiwinda na shindano hilo ambapo alisema warembo hao ni washindi wa vitongoji vya Miss Arusha city centre,Njiro ,Sakina pamoja na monduli.
Aidha alibainisha kawa ampaka sasa warembo wote wameingia kambini na wameshaanza mazoezi mbalimbali na anaimani kwa mwaka huu mrembo wa Reds miss Tanzania atatoka mkoani hapa.
"kwakeli sio najisifu ila warembo wetu ni wazuri na naimani watashinda maana wanaelimu ya kutosha na maadalizi ni mazuri kingine kikubwa mwaka huu mashindano haya yatakuwa ya tofauti sana kwani tumejipanga vilivyo na atutaki kufanyakosa kwanini kila siku taji liende dar na mwanza safari hii nitahakikisha linakuja arusha nawaaidi wakazi wa mkoa huu"alisema mwandago.
Aidha aliwataja baadhi ya vikundi ambayo vitatoa burudani kuwa ni pamoja na msanii mkubwa diamondi ambaye ndie amebeba tamasha zima ambaye atasindikizwa na kikundi cha ngoma na kucheza cha boda 2boda cha mkoani hapa,msichana sister p wa mkoa wa arusha ambaye ni mwimbaji wa miondoko ya rege kutoka jijini hapa huku akisema kuwa kunamsanii mungine mkubwa bado wapokwenye maongozi na wakishaingia mkataba atamtaja ni nani.
Aliwataja wadhamini wa shindano hilo kuwa ni Tbl kupitia kinywaji chake cha Reds,Tdl kupitia kinywaji chake cha dodoma win,Tanzanite one,mogaben priter,libeneke la kaskazini blog,Arusha traveling logde ambo ndio wametoa kambi ya warembo.
''kwa upande wa viingilio kutokana na hadhi ya onyesho hili ambalo litakuwa la kihistoria kwani kwanza kabisa linafanyika katika hotel ya nyota tano na msanii anavuma ndo anakuja kwa mara ya kwanza kwaiyo kiingilio kitakuwa VIP 50000 huku kawaida shilingi 30000 ila napenda kuwapa ofa wanafunzi ambao watakuwa wamjikusanya kama kikundi na kutoa taarifa vyuoni kwao kutakuwa na punguzo cha zaidi tuwasiliane mapema ili wajue"alibainisha Mwandago
Kwa upande wake mwalimu wa warembo hao Enjo Justice ambaye alishawahi kuwa mnyange wa mkoa wa mbeya mwaka 2005 pamoja na mrembo wa nyanda za juu kusini alisema kuwa mashindano hayo yanamanufaa kwakuwa sanaa ya urembo inatanuka siku hadi siku na wengi wanaangalia mfano kutoka kwao lakini inaitajika nidhamu kujitambua wewe ninani na unawakalisha kanda gani na hivyo ndivyo moja ya vigezo vya kujua mrembo anavyotakiwa kuwa.
Alisemakuwa pia mlengo ya mashindano haya na kuwafundisha warembo hawa ni pamoja na kutambua wao ni warembo na wanatakiwa kujitambua na kuwaelimisha jinsi ya kuipeperusha bendera hii ya urembo itambulike sehemu mbalimbali.

0 Comments:
Post a Comment
unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia