Ticker

6/recent/ticker-posts

RAIS WA ZAMANI WA LIBERIA AHUKUMIWA KIFUNGO CHA MIAKA 50 JELA

Mahakama Maalum ya Sierra Leone (SCS) Jumatano wiki hii imemhukumu kifungo cha miaka 50 jela Rais wa zamani wa Liberia, Charles Taylor baada ya kumtia hatiani kwa mashitaka 11 yaliyokuwa yanamkabili ikiwa ni pamoja na uhalifu wa kivita na uhalifu dhidi ya binadamu.

Majaji wa mahakama hiyo walikataa maombi yote ya kumpunguzia adhabuTaylor. Jaji Kiongozi wa katika kesi hiyo, Richard Lussick alisema kwamba ‘’ uongozi hauna budi kuendeshwa kwa kushughulikia uhalifu na siyo kwa kufanya uhalifu.’’

Muda mfupi baada ya hukumu hiyo kutolewa Wakili waTayloralitangaza kwamba atakata rufaa dhidi ya hukumu hiyo. Iwapo hukumu hiyo itadhibitishwa, adhabu hiyo ni sawa na kifungo cha maisha kwa Rais huyo wa zamani mwenye umri wa miaka 64.

Mahakama katika kumtia hatiani ilieleza kuwaTayloralilipatia kundi la waasi la RUF nchiniSierra Leonemisaada ya kijeshi, kioperesheni na fedha huku akijua kwamba walikuwa wanatenda uhalifu mkubwa ikiwa ni pamoja na mauaji, ubakaji,utumwa wa ngono,kuwasajili na kuwatumia watoto chini ya miaka 15 katika mapambano.

Mwendesha mashitaka alipendekeza adhabu ya kifungo cha miaka 80 jela.
Hukumu hiyo ilikuwa inatolewa toka mjini The Hague, Uholanzi na kurushwa moja kwa moja kwa mtandao wa intaneti.

Kesi yake ilianza kusikilizwa Juni 2007. Mwendesha mashitaka iliita mashahidi 94 wakiwemo 32 ambao walikuwa ni marafiki wa karibu waTaylorambao hatimaye walitoa ushahidi dhidi yake.

Tayloraliandaliwa mashitaka Juni 2003 lakini hati ya kukamatwa kwake ilibakia kuwa siri hadi alipokubali kuachia madaraka Agosti 2003, bada ya kupewa hifadhi ya ukimbizi wa kisiasa nchiniNigeria.
 Machi 2006, alitiwa mbaroni nchiniNigeriana kisha kusafirishwa hadi katika mahakama ya SCSL.
Serikali ya Uholanzi ilikubali kupokea kesi hiyo kusikiliziwa nchini mwake kufuatia ombi la Rais waLiberia, Ellen Johnson Sirleaf, ambaye alikuwa anahofia kuzuka kwa ghasia iwapo kesi hiyo ingesikilizwaSierra Leone.

Post a Comment

0 Comments