BENKI YA NMB KANDA YA KASKAZINI YAWAPA MAFUNZO WATEJA WAO



Meneja wa NMB kanda ya kaskazini,Vick Bishubu akifuatiwa na Mwenyekiti wa klabu ya wafanyabiashara wa NMB,Adam Shayo( kulia) j ,wakijumuika kumsikiliza kwa makini mtoa (hayupo pichani)katika semina ya siku moja kwa klabu ya wafanyabiashara wa NMB wa mkoa wa Arusha
Baadhi ya wanachama wa klabu ya wafanyabiashara wateja wa NMB wakifuatilia kwa makini mafunzo ya utafutaji masokob yaliyokuwa yakitolewa

Meneja wa NMB kanda ya kaskazini ,Vicky Bishibo wa pili kutoka kushoto akifuatilia kwa makini mafunzo ya ujasiriamali yaliyokuwa yakitolewa kwa klabu ya wafanyabaishara wa NMB ,katika hotel ya Golden Rose jijini Arusha
BENKI ya NMB kanda ya kaskazini imeanza  kutoa mafunzo ya ujasiriamali kwa wateja wake waliopo kwenye klabu ya wafanyanyabiashara  wa  NMB katika mikoa ya kanda ya kaskazini yanayolenga kuwajengea uwezo namna ya kutafuta masoko ili kuboresha biashara zao.

Meneja wa NMB kanda ya kaskazini , Vicky Bishubo aliyasema hayo wakati akifungua mafunzo ya siku moja kwa klabu ya wafanyabiashara wa NMB ,150 kutoka mkoa wa Arusha.

Alisema kuwa, mafunzo hayo yamekuwa yakiwasaidia kupata mbinu za kibiashara na fedha na kupanua uwezo katika utafutaji wa masoko na hivyo kuwawezesha kumudu urejeshaji  wa mikopo kwa wakati  pindi wanapokopa .

Bishubo alifafanua kuwa mafunzo hayo ,yamekuwa yakitolewa kila mwaka , yamesaidia kuwaunganisha wafanyabiashara na benki katika kupata mikopo na kuirejesha kwa wakati.

Aidha alisema mafunzo hayo yatatolewa pia kwa vilabu vya wateja wa NMB waliopo kwenye mikoa ya Kilimanjaro na Tanga wiki hii,ambapo vilabu vya benki hiyo kanda ya kaskazini vinawanachama zaidia 450 ambao wamekuwa wakinufaika na mafunzo hayo kila mwaka.

Naye mwenyekiti wa klabu ya wafanyabiashara wa NMB ,Adamu Shayo alisema kuwa mafunzo hayo yamewasaidia sana kuwajengea uwezo wa kibiashara kupanua wigo wa biashara zao ukizingatia nchi ya Tanzania sio kisiwa.

Alisema biashara zao zimekuwa zikiingiliana  na wenzao kote ulimwenguni katika kutafuta masoko ya ndani na nje,hivyo mafunzo kama hayo yatawasaidia kwa kiasi kikubwa kuwajengea uwezo wa kutafuta masoko.

Alisema kuwa mafunzo haya yamekuja wakati mwafaka kwa sababu mipaka ya Nchi za Afrika mashariki inafunguliwa na utandawazi unaenea kwa kasi na itasaidia kufaidika na soko la pamoja la jumuiya ya Afrika masharika.

Shayo ambaye ni mmiliki wa chuo cha ualimu Sila(Sila Teachers College) chenye namba ya usajili CU 115  kinachotoa cheti cha grade A ya ualimu na ajira moja kwa moja ndani ya serikali ,alisema ameweza kunufanika na mikopo ya benki ya NMB kupitia klabu ya wafanyabiashara na kuweza  kujenga chuo hicho chenye kiwango cha kimataifa.

Mafunzo hayo yateendelea kwenye mikoa ya Kilimanjaro ,Manyara na Tanga a,mbapo kwa kupitia vilabu vya wafanyabaishara,wateja wa NMB watapata fursa ya kupata mafunzo hayo .

About Woinde Shizza

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 Comments:

Post a Comment

unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia