WANANCHI WATAKIWA KUJITOKEZA KWA WINGI KUCHANGIA KATIBA NA SENSA

Serekali wilayani hai imetoa wito kwa wananchi wa wilaya hiyo kujitokeza kwa wingi wakati wa mchakato wa mjadala wa katiba pindi  tume  iliyoteuliwa na rais Jakaya mrisho Kikwete itakapofika wilayani humo

Hayo yalibainishwa na mkuu wa wilaya ya hai Novatus makunga wakati alipokuwa akiongea na polisi ili kusikiliza kero  mbalimbali zinazowakabili.

Akizungumza na polisi hao alisema kuwa kila mtanzania anayo haki ya kushiriki mjadala wa katiba na kutoa maoni yake wakati ukifika akiwemo polisi pamoja na wananchi wengine .

mkuu huyo wa wilaya alisisitiza kuwa katiba ya nchi siyo ya mtu mmoja ama kiongozi mmoja ama chama chochote cha siasa bali ni katiba ya watanzania wote kwa manufaa yao wote bila kujali itikadi za vyama vyoa vya siasa.

Aidha alisema kuwa kutokaana na hayo kila mwananchi ambaye  ni mtanzania anawajibu wa kushiriki katika mjadala huo na  ni fursa pekee ambayo rais ameitoa kwa watanzania .

Makunga akizungumzia swala la sensa  ya watu na makazi aliwataaka wananchi wa wilaya hiyo kujitokeza wote katika makazi yao ili waweze kuhesabiwa hapo ifikapo mwezi Agosti 26 mwaka huu huku akitoa wito kwa wannachi kutoa taarifa zote muhimu na sahii kutokana na maswali yaliyopo katika madodoso ya sensa.

Alibainisha kuwa sensa ya watu na makazi inaiwezesha kuandaa mipango ya maendeleo kwa uakini na usahii na kwa ubora zaidi katika kuleta maendeleo na tija kwa jamii na taifa kwa ujumla.

Aidha alibainisha kuwa sensa ya makazi na watu inawezesha serekali kutoa huduma kwa kwa wananchi wake zilizobora kutokana na kuwa na uhakikia na twakwimu za watu wake  juu ya mipango endelevu huku akitoa onyo kwa wananchi  kuepuka  kuwaficha watu wenye ulemavu wa aina yeyote kwani kundi hilo pia lina haki ya kuhudumiwa na serekali kama mwananchi mungine yeyote yule.

About Woinde Shizza

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 Comments:

Post a Comment

unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia