WATAKIWA KUTAFUTA UFUMBUZI WA KUZUIA WAKWEPA KODI

Naibu waziri wa sheria na katiba Angela Kairuki

WAKUU  wa idara mbalimbali za serikali kote nchini wameshauriwa  kutafuta ufumbuzi wa namna ya kudhibiti mianya ya ukwepaji kodi unaoisumbua serikali kwa muda mrefu.
Hayo yalisemwa naibu waziri wa sheria na katiba Angela Kairuki wakati akifungua mafunzo ya siku tano   ya kujadili  kuhusiana na ukusanyaji ya kodi kupitia mikata mbalimbali katika sekta za nishati ,madini na mafuta  ambayo inaendelea jijini hapa.
Alisema kwa muda mrefu Tanzania na hata nchi zingine za afrika mashariki na frika kwa ujumla imekuwa ikisumbuliwa na tatizo la ukwepaji kodi kutoka kwa makampuni makubwa ya uchimbaji wa madini na mafuta kupitia nyanja mbalimbali.
Kairuki alizitaja nyanja hizo zinazohusika na ukwepaji wa kosi hizo kuwa ni kupitia uhamisho wa makampuni hayo kwa kudai kuwa kampuni moja iliyopo Tanzania na tawi jingine nchi za nje kukwepa kulipa kodi kwa madai kuwa ilishalipa nchini humo.
“mafunzo haya pia yataisaidi kuwaongezea uwezo zaidi wataalamu hawa ambao wapo katika mafunzo haya na ninaimani kabisa tukitoka hapa kila mmoja ataendafanya kazi kama vile alivyopata mafunzo
Alisema kufanikiwa kupatikana kwa majibu ya namna ya kudhibiti mianya hiyo ya kodi kutawezesha nchi kunufaika na kodi hizo katika kuboresha sekta mbalimbali zikiwemo za elimu,maji,afya,miundo mbinu na nyingine nyingi.
Alisema uwezekano wa kupatikana kwa majibu hayo ni mkubwa kutokana na semina hiyo kuendeshwa na watu kutoka nchi zilizofanikiwa katika kupambana na tatizo hilo ambayo ni Marekani.
Sekta zinazoshiriki katika mafunzo hayo ni pamoja na mamlaka ya mapato Tanzania(TRA),Kituo cha uwekezaji cha taifa(TIC),Shirika la uagizaji wa mafuta(TPDC),Shirika la mazingira la taifa(MEM),Shirika la uchukuzi(MOT)Wizara ya fedha(MOF),Ofisi ya mwanasheria mkuu wa serikali bara na Zanzibar(AGC)Ofisi ya waziri mkuu(PMO) na Wizara ya mambo ya nje.
Semina hiyo ya siku tano ambayo ni ya tisa kufanyika hapa nchini inayoendelea mkoani hapa imeandaliwa na ofisi ya mwanasheria mkuu wa serikali chini ya ufadhili wa shirika la UNDP inayoongozwa na wakufunzi Stephen Shay na Edward Osterberg wote kutoka chuo kikuu cha Harvard cha nchini Marekani.

About Woinde Shizza

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 Comments:

Post a Comment

unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia