TAASISI YA KUKUZA SOKA ARUSHA YAJIVUNIA

TAASISI ya kulea na kuendeleza vipaji vya soka nchini ya Future Stars Academy iliyopo  jijini Arusha imejivunia kutoa wanasoka 6 kati ya 23 waliochaguliwa kujiunga na kambi ya Manchester United jijini Nairobi nchini Kenya mapema mwaka huu.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na mkurugenzi ambaye pia ni muasisi wa taasisi hiyo,Alfred Itaeli alisema kwamba taasisi yao inajivunia kutoa wachezaji hao ambao wawili  ni wasichana na wanne ni wavulana.

Aliwataja wasichana waliochaguliwa kujiunga na kambi hiyo kuwa ni pamoja na Irene Baisi na Jackline Gibson na kwa upande wa wanaume ni Suleman Yunus,Seleman Msemo,Rasali Mustafa pamoja na Anthony Angelo.

Itaeli ,alisema kwamba yeye kama muasisi ya taasisi hiyo anajisikia fahari kuwatoa wachezjai hao kwa kuwa ni heshima kwa mkoa wa Arusha na nchi kwa ujumla.

“Ni fahari kwa watoto na wana Arusha kwa ujumla wasichana hawa na kaka zao wamefanya kazi kubwa na kujituma sasa wanaweza kuuona wakijiamnini na kusonga mbele”alisema Itaeli

Hatahivyo,aliwapongeza baadhi ya wadau ambao wamejituma kuhakikisha taasisi hiyo inasimama hadi sasa hususani walimu wake,wazazi,watoto na wafadhili huku akisisitiza kwamba hiyo ni hatua chanya katika dira sahihi.

Vijana hao ni miongoni mwa vijana waliochaguliwa kuunda timu ya Tanzania kutoka michuano ya Airtel Rising Satrs na watajiunga katika kambi ya Manchester United jijini Nairobi  huku wakitarajia kupambana na  mataifa mengine 17 barani Afrika.

About Woinde Shizza

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 Comments:

Post a Comment

unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia