WATAKA KESI YA RUTO NA SANG KUANZA KUSIKILIZWA MACHI 2013

Mawakili wanaowatetea, Waziri wa Kenya, William Ruto na mwandishi wa habari  Joshua Sang Jumatatu waliiomba Mahakama ya Kimataifa ya Makosa ya Jinai (ICC) kuahirisha kuanza kusikilizwa kwa kesi yao hadi baada ya uchaguzi wa Rais nchini Kenya, unaopangwa kufanyika Machi 4, 2013.Upande wa mwendesha mashitaka haukupinga.
 
Mwendesha mashitaka, Florence Darques-Lane alisema hapingi kuanza kusikilizwa kwa kesi dhidi ya Wakenya hao katika kipindi cha miezi 10 ijayo lakini aliwaomba majaji kutoa maamuziyao ‘’bila kujali tarehe ya kufanyika kwa uchaguzi.’’

Aliwaomba pia majaji kuhakikisha ‘’bila kujali matokeo ya uchaguzi yatakuwaje, washitakiwa hao wahudhurie mahakamani wakati wa usikilizwaji wa kesiyao.’’

Washitakiwa hao wawili wanakabiliwa na mashitaka ya uhalifu dhidi ya binadamu kwa kudaiwa kuhusika kwao katika ghasia zilizotokea nchini mwao,baada ya uchaguzi wa rais Desemba 2007 ambapo watu kadhaa walipoteza maisha na wengine kukosa mahali pa kuishi.

Mwakilishi pekee wa waathirika wa ghasia hizo, Sureta Chana, alipinga kuahirisha kwa shaurihilokwa muda mrefu akidai kwamba wameshasubiri kwa zaidi ya miaka mitano kutendewa haki.’’Waathirika wanataka kupata tarehe ya kuanza kusikilizwa kwa shauri hili haraka iwezekanavyo,’’ aliiambia mahakama.’’
Nafikiri kuna kiwango fulani cha kuishiwa uvumilivu kwa upande wa watu ambao bado wanaendelea kuteseka kutokana na ghasia zilizotokea.’’  
  
Awali kabla ya kusikiliza hoja hizo,mawakili wa Ruto walielezea masikitoyaojuu ya kifo cha aliyekuwa Waziri wa Usalama waKenya, George Saitoti baada ya kuanguka kwa helikopta iliyombeba, Jumapili iliyopita na kuongeza kwamba alikuwa shahidi mtarajiwa katika kesi hiyo.

About Woinde Shizza

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 Comments:

Post a Comment

unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia